settings icon
share icon
Swali

Je! Tunatakiwa kutumia vyombo vya muziki kanisani?

Jibu


Vyombo vya muziki vilitumiwa kwa hakika katika ibada katika Agano la Kale (1 Mambo ya Nyakati 15:16, 16:42; 23:5; 2 Mambo ya Nyakati 7:6; 23:13; 29:26-27; 30:21; 34:12: Nehemia 12:36; Zaburi 4:1; 6:1, 54:1, 55:1, 61:1, 67:1, 76:1, Isaya 38:20; Amosi 6:5 Habakuki 3:19 ). Ukweli kwamba hakuna mahali Agano Jipya linakataa vyombo vya muziki inaonyesha kwamba mazoezi ya Agano la Kale yaliendelea katika kanisa la Agano Jipya. Kanisa la kwanza lilihusishwa karibu na Wayahudi. Ni uwezekano mkubwa sana kwamba waliendelea kutumia vyombo vya muziki katika kanisa, kama walivyofanya katika ibada zao za awali.

Kwa hiyo, hata bila kumbukumbu la wazi katika Agano Jipya, ni wazi kanisa linaweza kutumia vyombo vya muziki katika ibada yake. Hata hivyo, inawezekana kuna rejeleo katika Agano Jipya kwa vyombo vya muziki. Waefeso 5:19 inasema, "Mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu." Maneno "tenzi na nyimbo" ni tafsiri ya neno la Kiyunani psallontes, mzizi ambayo ulimaanisha "kusugua au kugusa" au "kusonga au kuvuta nyuzi." Ilikuwa kutumika kwa kawaida katika Giriki kutaja chombo cha kucheza muziki cha kamba. Kwa hali yoyote, Biblia haipingi au kuamuru matumizi ya vyombo vya muziki katika kanisa. Kwa hivyo, kanisa lina uhuru wa kuitumia au la kama inahisi kuongozwa na Mungu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Tunatakiwa kutumia vyombo vya muziki kanisani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries