settings icon
share icon
Swali

Biblia inasemaje kuhusu uzoefu wa kukaribia kifo?

Jibu


Uzoefu wa kukaribia kifo ni wakati mtu akiwa kando ya kifo na, baada ya kuponywa, huripoti tukio lisilo la kawaida, kwa kawaida uzoefu usio wa mwili au aina fulani ya maono ya mbinguni au kuzimu. Hakuna msaada maalum wa maandiko kwa uzoefu wa kukaribia kifo. Watu wengi hutumia 2 Wakorintho 12: 2-5 kama maandishi ya kibiblia ya uzoefu wa kukaribia kifo. Hata hivyo, hii inachukua uhuru mkubwa na ufafanuzi na inafanya dhana kwamba mtu (anadhani kuwa Paulo) alikuwa karibu na kifo au kwa kweli alikuwa amekufa wakati alijikuta mbinguni. Hakuna mahali ambapo kifungu hicho kinasema kuwa alikuwa au kukaribia kifo. Ilikuwa maono ambayo Mungu alimpa mtu kuhusu mbinguni, sio uzoefu wa kukaribia kifo.

Baada ya kusema hayo, si vigumu kwa Mungu kumpa mtu anayekaribia kifo, au mtu yeyote kwa jambo hilo, maono ya mbinguni. Hata hivyo, pamoja na kukamilika kwa uandishi wa kibiblia, maono sio uzoefu wa kawaida kwa Wakristo.

Tunahitaji kuwa makini sana katika namna tunavyothibitisha uzoefu wetu. Jaribio muhimu zaidi la uzoefu wowote ni kulinganisha hilo na Biblia. Shetani daima yuu tayari kusababisha udanganyifu na kupotosha mawazo ya watu. "Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao" (2 Wakorintho 11: 14-15).

Kwa sababu Biblia ii kimya kuhusu uzoefu wa kukaribia kifo, na uchunguzi wa kisayansi haujaweza kufanywa kwa uaminifu, hatuwezi kukubali uhalali wa uzoefu wa kukariba kifo kwa thamani ya juu juu. Ingekuwa imara sana kusema kwamba uzoefu wote wa kukariba kifo ni uigizo, hufikiriwa, au wa kishetani, lakini bado kuna wasiwasi mkubwa, Kibiblia, juu ya uhalali wa uzoefu wa kukaribia kifo. Tena, ufafanuzi wowote wa uzoefu wa kukaribia kifo unapaswa kuthibitishwa dhidi ya ukweli wa Maandiko. Uzoefu kama huo unatoka kwa Mungu, utakuwa unaohusishwa na kile ambacho tayari amekifunua katika Neno Lake na hatimaye huleta utukufu kwake kwa jina la Yesu Kristo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasemaje kuhusu uzoefu wa kukaribia kifo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries