settings icon
share icon
Swali

Je! Biblia inasema nini kuhusu uuzaji kanisani?

Jibu


Maandiko ya kwanza yanayokuja akilini kuhusu kuuza ndani ya kanisa ni Mathayo 21: 12-13, Marko 11: 15-17, Luka 19: 45-46, na Yohana 2: 13-17, zote ambazo zinaelezea matukio (kuwa yalikuwa mawili) wakati Yesu "alitakasa" hekalu. Wakati Aliona aina ya shughuli ambazo zilikuwa zinafanyika katika nyumba ya Baba Yake, alikasirika sana. Kwa wazi, hiki sio kile hekalu lilijengewa.

Yesu aliwachukulia wafanyabiashara na wateja kuwa na hatia ya kuchafua hekalu. Bidhaa vilivyonunuliwa na kuuzwa vilijumuisha wanyama wa dhabihu (Yohana 2:14). Pia walikuwepo wale waliobadilishana sarafu moja na nyingine. Hii ilihitajika kwa sababu sarafu za Kirumi na aina zingine za sarafu zilionekana kuwa hazikubaliki kwa matoleo ya hekaluni. Hekalu ilikuwa ni mahali ambapo Mungu alikutana na watu wake. Kuifanya kuwa mahali pa kuuza ilikuwa inazuia ibada, na haswa kuchukua nafasi ambayo ilikuwa imetengewa watu wa mataifa kuabudu. Ni dhahiri, wafanyabiashara na wabadilishanaji wa pesa walikuwa wakitoza viwango vya kupindukia kiwango kwamba hekalu ikiwa ni soko la wezi (Mathayo 21:13).

Ni wazi, kuuza vitabu, kuwa na bahati nasibu, kuwa na mchango, nk, ni tofauti na kile kilichokuwa kikiendelea hekaluni. Yesu hakukasirishwa kwamba walikuwa wakiuza hekaluni, lakini badala yake uuzaji ilikuwa lengo badala ya Mungu. Yesu pia alikasirishwa kwa sababu wabadilishanaji fedha walikuwa wakiwatumia watu vibaya, ambao wengi wao walikuwa masikini, ambao walihitaji huduma yao. Njiwa na wanyama wengine walihitajika kwa matoleo, na zaka za pesa zilizokubalika pia zilihitajika.

Hiyo siyo hali katika makanisa ya hii leo. Ununuzi katika duka la vitabu vya kanisa au katika uuzaji wa usanii kanisani, kama mfano, ni kwa hiari kabisa. Hakuna ununuzi unaohitajika ili mtu auhudhurie ibada. Ikiwa kanisa litaamua kuuza kitu ndani ya kanisa au kuwa mchango wa fedha, inapaswa kuhakikisha kuwa uuzaji huo haupokei uangalifu usiofaa na haupotoshi ibada na mafundisho ya Neno la Mungu. Uuzaji haupaswi kamwe kufanywa kuwa wa "shinikizo."

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Biblia inasema nini kuhusu uuzaji kanisani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries