settings icon
share icon
Swali

Kwa nini Yesu aliwaagiza watu wasiambie wengine kuhusu miujiza aliyotenda?

Jibu


Baada ya kumponya mtu wa ukoma (Marko 1: 41-42), "Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwambia; 'Angalia usimwambie mtu yeyote jambo hili ...'" (Marko 1:43) -44). Kwa njia yetu ya kufikiria, inaonekana kwamba Yesu angehitaji kila mtu kujua kuhusu muujiza. Lakini Yesu alijua kwamba utangazaji juu ya miujiza hiyo inaweza kuzuia kazi yake na kupotosha uma kutoka kwa ujumbe Wake. Mariko aliandika kumbukumbu kwamba hii ndio hasa kilichotokea. Katika msisimko wa mtu huyu juu ya kuponywa kwa miujiza, hakumtii. Matokeo yake, Kristo aliamua kuhamisha huduma yake mbali na mji na katika mikoa ya jangwa (Marko 1:45) "Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote wasiwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande."

Zaidi ya hayo, Kristo, ingawa alikuwa amemtakasa mwenye ukoma, bado alimtaka awe amtiivu kwa sheria za nchi — enenda mara moja kwa kuhani, na usikawie kuacha kuzungumza juu ya kuponywa kwake. Inawezekana pia kwamba, ikiwa hakutaka kwenda mara moja, watu wenye mawazo mabaya wataenda mbele yake na kumdanganya kuhani na kuzuia kutangazwa kuwa aponywa kwa sababu ulifanywa na Yesu. Ilikuwa ya umuhimu zaidi kama kuhani aliutangaza kuwa ni tiba ya kweli, kwamba kunaweza kuwa hakuna ubaguzi kati ya Wayahudi dhidi ya kuwa ni muujiza wa kweli.

Hatimaye, Yesu hakutaka watu kuzingatia miujiza aliyoifanya, badala yake ujumbe aliotangaza na kifo alichokufa. Vivyo hivyo ilivyo hii leo. Mungu angependa tuangazie muujiza wa uponyaji wa wokovu kupitia Yesu Kristo badala ya kuzingatia uponyaji mwingine na / au miujiza.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kwa nini Yesu aliwaagiza watu wasiambie wengine kuhusu miujiza aliyotenda?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries