settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kuwa shahidi bora wa Kristo katika ulimwengu uliopotea?

Jibu


"Shahidi" ni mtu anayeshuhudia ukweli, hivyo ili uwe ushahidi bora kwa Kristo, mtu lazima awe na ujuzi wa kwanza juu yake. Yohana Mtume anasema hivi katika 1 Yohana 1: 1-3, wakati anasema, "Lileā€¦, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima; (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu); hilo tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na." Leo hii, sisi ambao tulipata maisha mapya katika Kristo tunatoa taarifa ya upendo na msamaha wake, zote mbili kwa maneno na kwa njia tunayoishi maisha yetu. Hii ni kushuhudia. Ili kuwa na ufanisi katika ushuhuda wetu, tunapaswa kukumbuka mambo kadhaa ya msingi:

1) Mada ya ushahidi wetu ni Yesu Kristo. Paulo alifafanua Injili kama kifo, kuzika, na ufufuo wa Yesu Kristo (1 Wakorintho 15: 1-4). Ikiwa hatuelezei dhabihu ya Kristo, basi hatuwezi kugawana injili. (Ona pia 1 Wakorintho 2: 2 na Waroma 10: 9-10.) Sehemu muhimu ya mada hii ni ukweli kwamba Yesu Kristo ndiye njia pekee ya wokovu, sio njia moja tu. "Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi" (Yohana 14: 6, msisitizo aliongezwa).

2) Nguvu ya ushuhuda wetu ni Roho Mtakatifu. Ni Roho ambaye hubadilisha maisha (Tito 3: 5), na maisha yaliyobadilishwa ni dhahiri kwa wote. Tunaposhuhudia, tunapaswa kutumia muda mwingi katika sala, tunapaswa kuidhinisha nguvu za Roho ili tuwezeshwe kuacha nuru yetu iangaze kwa njia ambayo wengine watatambua uwezo wa Mungu ndani yetu (Mathayo 5:16).

3) Utibitisho wa ushahidi wetu utaonyeshwa jinsi tunavyoishi maisha yetu. Wafilipi 2:15 huweka lengo hili kwetu: "mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu." Shahidi wa Kikristo ataishi maisha yake juu ya madai kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, ambaye matunda yake tunayoonyesha wakati tunapokaa katika Kristo (Yohana 15: 1-8; Wagalatia 5: 22-23).

Labda muhimu zaidi, tunapaswa kuwa na ujuzi wa kutosha wa Maandiko ili tuweze kuwasilisha injili kwa wengine kwa usahihi na kwa uuwiano. "Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu" (1 Petro 3:15). Daima kuwa tayari humaanisha kujifunza Biblia kwa bidii, kukumbuka Maandiko, na kuomba fursa zilizopewa na Mungu kugawana na wale ambao mioyo yao imeandaliwa na Bwana kuusikia ujumbe wake wa wokovu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kuwa shahidi bora wa Kristo katika ulimwengu uliopotea?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries