settings icon
share icon
Swali

Ukomavu wa kiroho ni nini? nawezaje kuwa mkomavu kiroho zaidi?

Jibu


Ukomavu wa Kiroho unaweza kuafikiwa kwa kukua zaidi kama Yesu Kristo. Baada ya kuoka, kila Mkristo anaanza mchakato wa kukua kiroho, akiwa na nia ya kukomaa kiroho. Kulingana na mtume Paulo, ni hali inayoendelea ambayo haiwezi kuishia katika maisha haya. Katika Wafilipi 3: 12-14, akizungumzia ufahamu kamili wa Kristo, anawaambia wasomaji wake kuwa yeye mwenyewe "Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu." Kama Paulo, sisi pia tunapaswa kukaza mbele kuelekea kwa ufahamu wa Mungu katika Kristo.

Ukomavu wa Kikristo unamhitaji mtu kurekebisha vipaumbele vyake, kubadilika kutoka kujifurahisha mwenyewe hadi kumpendeza Mungu na kujifunza kumtii. La muhimu katika ukomavu ni kuwa thabiti, na mvumilivu katika kufanya mambo ambayo tunajua yatatusongesha karibu na Mungu. Mambo kama haya yanajulikana kwetu kama vigezo vya kiroho na ni pamoja na mambo kama vile kusoma Biblia, sala, ushirika, huduma, na usimamishi. Haijalishi jitihada zetu katika mambo hayo, ijapokuwa hakuna kati ya haya itawezekana bila kuwezeshwa na Roho Mtakatifu ndani yetu. Wagalatia 5:16 inatuambia kwamba tunapaswa 'tutembee kwa Roho.' Neno la Kiyunani ambalo linatumika hapa kwa niapa ni "kutembea" hakika linamaanisha "kutembea kwa lengo, na kwa mtazamo." Baadaye katika sura hiyo hiyo, Paulo anatuambia pia tunapaswa "kutembea kwa Roho." Hapa, neno lililotafsiriwa "kutembea" lina dhana ya kuchukua vitu "hatua kwa hatua, hatua moja kwa wakati fulani." Ni kujifunza kutembea chini ya mafundisho ya mwingine — Roho Mtakatifu. Kujazwa na Roho inamaanisha kuwa sisi tunatembea chini ya uongozi wa Roho. Tunaponyenyekea zaidi na zaidi kwa uongozi wa Roho, tutaona pia ukuaji wa matunda ya Roho katika maisha yetu (Wagalatia 5: 22-23). Hii ndio sufa ya kukomaa kiroho.

Tunapokuwa Wakristo, tunapewa yale yote tunayohitaji ili kukomaa kiroho. Petro anatuambia kwamba " Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe." (2 Petro 1: 3). Mungu pekee ndiye chanzo chetu, na ukuaji wote huja kwa neema kupitia kwake, lakini tunawajibika kufanya uamuzi wa kumtii. Petro anatusaidia tena katika eneo hili: "Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa, na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo. Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo. "(2 Petro 1: 5-8). Kuwa na matokeo na kuzaa matunda katika kumfahamu Bwana Yesu ndicho kiini cha kukua kiroho.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ukomavu wa kiroho ni nini? nawezaje kuwa mkomavu kiroho zaidi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries