settings icon
share icon
Swali

Je, ni makosa kuwa na uhusiano na jamaa wa karibu?

Jibu


Mahusiano ambayo Mungu aliyazuia katika Sheria ya Agano la Kale yaliorodheshwa katika Walawi 18: 6-18. Katika kifungu hicho, Waisraeli waliamriwa wasiolewe mwazi kwa mzazi, mjukuu .Ndugu au dada wa mzazi (yaani, shangazi au mjomba), au ndugu wa nusu. Ndoa kati ya binamu haipo popote katika Biblia.

Katika siku za mwanzo sana za ubinadamu, kulikuwa na idadi ndogo ya wanadamu. Matokeo yake, ndoa kati ya jamaa wa karibu mara nyingi ilikuwa muhimu. Haikuwa mpaka ubinadamu uliongezeka sana duniani kwamba watu hawakuhitajika kuoana kati ya jamaa. Katika siku za mwanzo za ubinadamu, kanuni za maumbile za kibinadamu haikuharibiwa kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na leo. Kwa hiyo, ilikuwa salama kwa jamaa wa karibu kuolewa na kuwa na watoto. Kulikuwa na hatari ndogo ya kusababishwa hitilafu za maumbile kwa watoto wao. Mara tu idadi ya watu ilipopanuka na kwa sababu ya dhambi, kanuni za maumbile za kibinadamu ziliharibiwa sana, Mungu aliamuru dhidi ya ndoa ya jamaa wa karibu.

Kwa hiyo hakuna kitu kimsingi kibaya juu ya kuoa ndugu wa karibu. Sababu ambayo hatupaswi kuifanya hivyo ni kwamba inasababisha hitilafu za maumbile. Zaidi ya hayo, mataifa mengi leo yana sheria kali dhidi ya ndoa kati ya jamaa wa karibu. Biblia inatuamuru kuitii sheria za taifa tunaloishi (Warumi 13: 1-6). Sheria nyingi hutambua binamu wa pili kwa kuwa tofauti ili kuruhusu ndoa. Wanandoa wowote wanaohusiana na kuzingatia ndoa wanapaswa kuomba kwa moyo wote kwa Mungu kuwapa hekima na busara ili kupata kujua mapenzi Yake (Yakobo 1: 5). Wanandoa wanapaswa kuwasiliana na familia zao kuhusu jambo hili, pia.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni makosa kuwa na uhusiano na jamaa wa karibu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries