settings icon
share icon
Swali

Je, mashahidi wawili katika kitabu cha Ufunuo ni akina nani?

Jibu


Kuna mitazamo mitatu ya msingi juu ya utambulisho wa mashahidi wawili katika Ufunuo 11: 3-12: 1) Musa na Eliya, 2) Henoki na Eliya, na 3) Waumini wawili wasiojulikana ambao Mungu anawaita kuwa mashahidi wake nyakati za mwisho.

Musa na Eliya wanaonekana kuwa ni wao mashahidi kutokana na uwezo wa kugeuza maji kuwa damu (Ufunuo 11: 6), ambayo kwayo Musa anajulikana (Kutoka sura ya 7); na uwezo wao wa kuwaangamiza watu kwa moto kutoka mbinguni (Ufunuo 11: 5), ambayo kwayo Eliya anajulikana (2 Wafalme sura ya 1). Pia kutoa nguvu kwa mtazamo huu ni ukweli kwamba Musa na Eliya walionekana pamoja na Yesu wakati wa ufufuo (Mathayo 17: 3-4). Zaidi ya hayo, tamaduni za Kiyahudi zinatarajia Musa na Eliya kurudi baadaye. Malaki 4: 5 inatabiri kuja kwa Eliya, na Imani ya Wayahudi wengine kwamba ahadi ya Mungu ya kumfufua nabii kama Musa (Kumbukumbu la Torati 18:15, 18) inaashiria kurudi kwa Musa, pia.

Henoki na Eliya huonekana kuwa hao mashahidi wawili kwa sababu hao ndio watu wawili katika historia ambao hawakuwahi kukumbana na kifo (Mwanzo 5:24; 2 Wafalme 2:11). Ukweli kwamba Henoki na Eliya hakuna aliyekufa inaonekana kuwa wanastahili kufananishwa, kufa na kufufuliwa kwa mashahidi wawili (Ufunuo 11: 7-12). Washiriki wa maoni haya wanakiri kuwa Waebrania 9:27 (watu wote hufa mara moja) inamtoa Musa kuwa mmoja wa mashahidi hao wawili, kwa kuwa Musa alikuwa amekufa mara moja tayari (Kumbukumbu la Torati 34: 5). Hata hivyo, kuna wengine kadhaa katika Biblia ambao walikufa mara mbili-k.m., Lazaro, Dorkasi, na binti wa Yairo-kwa hivyo hakuna sababu yoyote ya Musa kuondolewa kwa huo msingi.

Mtazamo wa tatu kimsingi unasema kuwa Ufunuo sura ya 11 haijalihusisha jina lolote maarufu kwa mashahidi hao wawili. Ikiwa mashahidi hao walikuwa Musa na Eliya, au Henoki na Eliya, kwa nini Maandiko yangekuwa kimya kuwatambulisha? Mungu ana uwezo wa kuchukua waumini wawili wa kawaida na kuwawezesha kufanya ishara sawa na maajabu kama Musa na Eliya. Hakuna kitu katika Ufunuo 11 kinachohitaji sisi kuchukua sifa maarufu kwa mashahidi hao wawili.

Mtazamo upi ni sahihi? Hatujui kwa hakika. Udhaifu wa mtazamo wa kwanza ni kwamba Musa alikuwa amekufa mara moja tayari na kwa hivyo hawezi kuwa mmoja wa mashahidi hao wawili ( kwa kuwa kifo chake kitakuwa kinyume na Waebrania 9:27); hata hivyo, walio na mtazamo huu watasema kwamba watu wote ambao walifufuliwa kwa muujiza katika Biblia (k.m., Lazaro) baadaye walikufa tena. Waebrania 9:27 inaweza kuonekana kama "sheria ya kawaida" na si kanuni halisi. Kwa utabiri wa Biblia wa kuja kwa Eliya na nabii kama Musa, Agano Jipya linaonyesha wazi kwamba unabii huo ulitimizwa na Yohana Mbatizaji na Yesu mwenyewe, kwa mtiririko huo.

Hakuna udhaifu wazi kwa mtazamo wa pili wa Henoki na Eliya, kwa vile hutatua tatizo la kufa mara moja. Ina maana kwamba pengine Mungu aliweza kuwachukua Henoki na Eliya mbinguni bila kufa ili "kuwaokoa" kwa kusudi maalum baadaye. Pia hakuna udhaifu wazi kwa mtazamo wa tatu.

Mitazamo yote mitatu ni tafsiri iliyoeleweka, lakini hatuwezi kuwa na hakika kabisa juu ya yoyote kati yao kwa kuwa Biblia haijawatambulisha mashahidi hao. Kwa hivyo Wakristo hawapaswi kuzingatia suala hili.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, mashahidi wawili katika kitabu cha Ufunuo ni akina nani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries