settings icon
share icon
Swali

Ni nini ishara ya ubatizo wa maji?

Jibu


Ubatizo wa maji huashiria imani kamili ya muumini na kumtegemea kabisa kwa Bwana Yesu Kristo, pamoja na kujitolea kuishi kwa utii kwake. Pia inaonyesha umoja na watakatifu wote (Waefeso 2:19), yaani, na kila mtu katika kila taifa duniani ambaye ni mwanachama wa Mwili wa Kristo (Wagalatia 3: 27-28). Ubatizo wa maji huonyesha haya na zaidi, lakini sio ubatizo unatuokoa. Badala yake, tunaokolewa na neema kupitia imani, sio kwa kazi nzuri tunazotenda (Waefeso 2: 8-9). Tunabatizwa kwa sababu Bwana wetu aliamuru: "Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu" (Mathayo 28:19).

Ubatizo wa maji ni wa waumini. Kabla ya kubatizwa, lazima tuamini kwamba sisi ni wenye dhambi wanaohitaji wokovu (Warumi 3:23). Tunapaswa pia kuamini kwamba Kristo alikufa msalabani kulipa dhambi zetu, kwamba alizikwa, na kwamba alifufuliwa ili kutuhakikisha mahali petu mbinguni (1 Wakorintho 15: 1-4). Tunapogeuka kwa Yesu, kumwomba msamaha wa dhambi zetu na kuwa Bwana na Mwokozi wetu, tumezaliwa tena kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Uokoaji wetu wa milele ni wa uhakika, na tunaanza kuifia nafsi zetu na kumuishia Kristo (1 Petro 1: 3-5). Wakati huo sisi tumehitimu kimaandiko kubatizwa.

Ubatizo wa maji ni picha nzuri ya kile Bwana wetu ametufanyia. Tunapozikwa kabisa ndani ya maji, tunaashiria kuzikwa kwa Bwana wetu; tunabatizwa katika kifo chake msalabani na sisi si watumwa wa nafsi au dhambi (Warumi 6: 3-7). Wakati tunapofufuliwa kutoka kwa maji, kiishara tumefufuliwa-kufufuliwa kwenye maisha mapya katika Kristo kuwa na Yeye milele, kuzaliwa katika familia ya Mungu wetu mwenye upendo (Waroma 8:16). Ubatizo wa maji pia unaonyesha utakaso wa kiroho tunaopata tunapookolewa; kama vile maji husafisha mwili, hivyo Roho Mtakatifu hutakasa mioyo yetu tunapomwamini Kristo.

Ukweli kwamba ubatizo wa maji sio lazima kwa ajili ya wokovu unaonekana vizuri katika mfano wa mtu aliyeokolewa ambaye hakubatizwa katika maji-wahalifu msalabani (Luka 23: 39-43). Mtu mwenye dhambi aliyekubali mwenyewe alikiri Yesu kama Bwana wake akiwa anakufa msalabani karibu Naye. Mwizi aliomba wokovu na kusamehewa dhambi zake. Ingawa hakuwa na ubatizo wa maji kamwe, wakati huo alikuwa amebatizwa kiroho katika kifo cha Kristo, na kisha akafufuliwa kwenda uzima wa milele kwa nguvu ya neno la Kristo (Waebrania 1: 3).

Wakristo wanapaswa kubatizwa nje ya utii na upendo kwa Bwana wetu Yesu (Yohana 14:15). Ubatizo wa maji kwa kuzamizwa ni njia ya kibiblia ya kubatizwa kwa sababu ya uwakilishi wa mfano wa kifo, kuzikwa, na ufufuo wa Kristo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni nini ishara ya ubatizo wa maji?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries