settings icon
share icon
Swali

Ni vitu gani hapa duniani vina thamani ya kweli ya milele?

Jibu


Inakwenda bila kusema kuwa vitu pekee vya thamani ya milele katika ulimwengu huu ni vile vya milele. Maisha katika ulimwengu huu ni ya muda, si ya milele, na kwa hivyo, sehemu pekee ya uzima ambayo ina thamani ya milele ni ile inadumu kwa milele. Kwa hakika, jambo muhimu zaidi katika dunia hii ambayo ina thamani ya milele ya kweli ni kuwa na uhusiano na Yesu Kristo, kama zawadi ya bure ya uzima wa milele inakuja kwa njia ya Yeye tu kwa wote ambao wanaoamini (Yohana 3:16). Vile Yesu alisema, "Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi"(Yohana 14:6). Kila mtu ataenda kukaa mahali fulani kwa milele yote, Wakristo na wasio Wakristo sawa. Na hatima ya pekee ya milele isipokuwa ile ya mbinguni pamoja na Kristo ni moja ambayo hutoa adhabu ya milele kwa wale ambao wanaomkataa Yeye (Mathayo 25:46).

Kuhusu mambo mengi ya kimwili ambayo ulimwengu hutoa, ambayo wengi hung'ang'ana kutafuta, Yesu alitufundisha sisi kutohifadhi kwa nafsi zetu wenyewe hazina za ulimwengu ambazo zinaweza kuharibiwa au kuibiwa (Mathayo 6:19-20). Baada ya yote, hatukuleta kitu katika ulimwengu huu, na hatuwezi kuchukua chochote kutoka kwake. Bado maadili yetu ya msingi ya Kikristo mara nyingi hutilia maanani katika jitihada zetu za kutafuta mafanikio na faraja ya kimwili, na katikati ya shughuli hizi za kidunia sisi mara nyingi tunasahau kuhusu Mungu. Musa alizungumzia jambo hili miaka 3,500 iliyopita vile watu wake walikuwa karibu kuingia katika Nchi ya Ahadi. Aliwaonya wasisahau kuhusu Mungu, kwa maana alijua mara moja wao "walijenga nyumba nzuri na kuishi" mioyo yao ingekuwa na kiburi na wangeweza kusahau juu Yake (Kumbukumbu la Torati 8:12-14). Hakika hakuna thamani ya milele katika kuishi maisha yetu kwa ajili yetu wenyewe, kutafuta kupata katika maisha yote tunayoweza, kama mfumo wa ulimwengu ungeweza kutufanya kuamini.

Bado kunaweza kuwa thamani kubwa ya milele katika kile tunachofanya na maisha yetu wakati wa muda mfupi sana tuko hapa duniani. Ingawa Maandiko yanasema wazi kwamba matendo yetu mema ya duniani hayatatuokoa au kutuweka salama (Waefeso 2:8-9), ni sawa wazi kwamba tutapata malipo ya milele kulingana na kile tumefanya wakati hapa duniani. Kama Kristo mwenyewe alisema, "Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake" (Mathayo 16:27). Hakika, Wakristo ni "... kazi ya yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo" (Waefeso 2:10, msisitizo aliongezwa). Haya "matendo mema" yanahusiana na kumtumikia Bwana kwa ubora tunaoweza na kile alichotupa na kwa utegemezi kamili juu Yake.

Mtume Paulo anazungumzia ubora wa kazi ambazo zinaweza kuleta tuzo za milele. Kulinganisha Wakristo na "wajenzi" na ubora wa kazi zetu na vifaa vya ujenzi, Paulo anatujulisha kwamba vifaa vyema vinavyoweza kupona moto wa Mungu na kuwa na thamani ya milele ni "dhahabu, fedha, na mawe ya gharama kubwa," kwa kuwa kutumia vifaa duni "Mbao, nyasi kavu na majani makavu" kujenga juu ya msingi ambao ni Kristo haina thamani ya milele na haiwezi kulipwa (1 Wakorintho 3:11-13). Kwa kweli, Paulo anatuambia kwamba sio mwenendo wetu wote na kazi zitakazostahili tuzo.

Kuna njia nyingi ambazo huduma yetu kwa Bwana itatuletea tuzo. Kwanza, tunahitaji kutambua kwamba kila muumini wa kweli ametengwa na Mungu na kwa Mungu. Tulipopokea zawadi ya Mungu ya wokovu, tulipewa zawadi fulani za kiroho (1 Wakorintho 12:7, 11). Na ikiwa tunadhani zawadi zetu si za maana, tunahitaji kukumbuka kwamba, kama Paulo alivyoambia kanisa la Korintho, mwili wa Kristo umeundwa na sehemu nyingi (1 Wakorintho 12:14). Na "Bali Mungu amevitia viuongo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. . . na vile viuongo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge Zaidi vyahitajiwa zaidi"(1 Wakorintho 12:18, 22 msisitizo aliongeza). Ikiwa unatumia zawadi zako za kiroho, unashiriki nafasi muhimu katika mwili wa Kristo na kufanya kile ambacho kina thamani ya milele.

Kila mwanachama wa mwili wa Kristo anaweza kutoa michango yenye manufaa tunapotafuta kwa unyenyekevu kuimarisha mwili na kumtukuza Mungu. Hakika, kila kitu kidogo kinaweza kuongeza kwenye nakshi nzuri ya kile Mungu anachoweza kufanya wakati sisi kila mmoja tutafanya sehemu yetu. Kumbuka, duniani Kristo hana mwili lakini ni yetu, hakuna mikono lakini yetu, na hakuna miguu lakini yetu. Zawadi za kiroho ni njia ya Mungu ya kutoa neema Yake kwa wengine. Tunapoonyesha upendo wetu kwa Mungu kwa kutii amri Zake, tunapovumilia katika imani licha ya upinzani wote na mateso yote, wakati kwa jina Lake tunaonyesha huruma kwa maskini na wagonjwa na wasio na bahati, na wakati tunapunguza maumivu na mateso ambayo yanatuzunguka sisi, basi kwa hakika tunajenga na "dhahabu, fedha, na mawe ya gharama kubwa" ambayo yana thamani ya kweli ya milele.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni vitu gani hapa duniani vina thamani ya kweli ya milele?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries