settings icon
share icon
Swali

Nini maana na umuhimu wa taji ya miiba?

Jibu


Baada ya majaribio ya kuzingiziwa ya Yesu na baadaye kuchapwa mijeledi, na kabla ya kusulubiwa, askari wa Kirumi "wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, salamu, Mfalme wa Wayahudi" (Mathayo 27:29; tazama pia Yohana 19:2-5). Wakati taji ya miiba ingekuwa chungu sana, taji ya miiba ilikuwa zaidi juu ya dhihaka kuliko ilivyokuwa juu ya maumivu. Hapa alikuwa "Mfalme wa Wayahudi" akipigwa, kutemewa mate, na kutukanwa na askari wa Kirumi wanaokisiwa kuwa wa ngazi ya chini. Taji ya miiba ilikuwa kukamilisha dhihaka yao, kuchukua ishara ya kifalme na utukufu, taji, na kuibadilisha kuwa kitu chungu na cha kushusha hadhi.

Kwa Wakristo, taji ya miiba ni kumbusho la mambo mawili: (1) Yesu alikuwa, na ni mfalme kwa kweli. Siku moja, ulimwengu wote utasujudu kwa Yesu kama "Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana" (Ufunuo 19:16). Kile askari wa Kirumi walimaanisha kama dhihaka, kwa kweli ilikuwa ni picha ya nafasi mbili za Kristo, kwanza ya mtumishi wa kuteseka (Isaya 53), na pili ya Masihi mshindi-Mfalme (Ufunuo 19). (2) Yesu alikuwa tayari kuvumilia maumivu, matusi, na aibu, yote kwa akaunti yetu. Taji ya miiba, na mateso yaliyoambatana pamoja nayo, yaliisha kitambo, na sasa Yesu amepokea taji ambalo anastahili. "Ila twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu" (Waebrania 2: 9, msisitizo aliongeza).

Kuna mfano zaidi unaoonekana katika taji ya miiba. Wakati Adamu na Hawa walifanya dhambi, walileta mabaya na laana juu ya ulimwengu, sehemu ya laana juu ya ubinadamu ilikuwa "... ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na miiba itakuzalia ... "(Mwanzo 3: 17-18, msisitizo uliongeza). Askari wa Kirumi bila kujua walichukua kitu cha laana na kuifanya kuwa taji kwa yule atakaye kutuokoa kutoka kwa laana hiyo. "Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti" (Wagalatia 3:13). Kristo, katika dhabihu yake ya upatanisho kamili, alitukomboa kutoka kwa laana ya dhambi, ambayo mwiba ni ishara. Wakati ilipangwa kuwa dhihaka, taji ya miiba ilikuwa, kwa kweli, ishara bora ya Yesu ni nani na kile alichokuja kukamilisha.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nini maana na umuhimu wa taji ya miiba?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries