settings icon
share icon
Swali

Je, somo la malaika ni lini?

Jibu


Aloilojia ni utafiti wa malaika. Kuna maoni mengi yasiyo ya kibiblia ya malaika hii leo. Baadhi wanaamini kwamba malaika ni wanadamu ambao wamekufa. Wengine wanaamini kwamba malaika ni vyanzo vyenye nguvu. Wengine bado wanakataa kuwepo kwa malaika kabisa. Eleo la kibiblia la utafiti wa malaika utakosoa imani hizi za uwongo. Utafiti wa malaika unatuambia kile Biblia inasema juu ya malaika. Ni utafiti wa jinsi malaika wanavyohusiana na ubinadamu na kumtumikia makusudi ya Mungu. Hapa kuna maswala muhimu katika utafiti wa malaika:

Biblia inasema nini kuhusu malaika? Malaika ni viumbe tofauti kabisa kutoka kwa wanadamu. Wanadamu hawakui malaika baada ya kufa. Malaika kamwe hawajawai kuwa na kamwe,hakuwa, wanadamu. Mungu aliwaumba malaika, kama alivyoumba binadamu.

Je, malaika ni wa kiume au kike? Biblia has haiunga mkono jinsia ya malaika kuwa ya kiume au kike. Kila wakati malaika "hupewa" jinsia katika Maandiko, huwa ni ya kiume (Mwanzo 19: 10,12; Ufunuo 7: 2; 8: 3; 10: 7), na majina pekee yaliyotajwa ya malaika ni Mikaeli na Gabrieli, kwa ujumla huchukuliwa kuwa majina ya kiume.

Je, tuna malaika wa ulinzi? Hamna shaka kwamba malaika wema husaidia kulinda waumini, kufunua habari, kuongoza watu, na kwa ujumla, kuwahudumia watoto wa Mungu. Swali ngumu ni ikiwa kila mtu au kila muumini amewekewa malaika wake.

Nani / Malaika wa Bwana ni nani? Utambulisho sahihi wa "malaika wa Bwana" haujaoneswha katika Biblia. Hata hivyo, kuna "vigezo" muhimu muhimu kuhusu utambulisho wake.

Makerubi ni nani? Je, kerubi ni malaika? Makerubi ni viumbe wa malaika wanaohusika katika ibada na sifa za Mungu. Zaidi ya kuimba sifa za Mungu, pia hutumikia kama ukumbusho dhahiri wa ukuu na utukufu wa Mungu na uwepo wake katika kwa watu wake.

Maserafi ni nani? Je, ni malaika wa Sarufi? Isaya sura ya 6 ndio mahali pekee katika Biblia ambayo inazungumzia hasa Maserafi. Maserafi ("moto, moto uchomao") ni malaika viumbe wanaohusishwa na maono ya nabii Isaya kuhusu Mungu katika hekalu.

Utafiti wa malaika hutupa mtazamo wa Mungu wa malaika. Malaika ni wanadamu ambao wanaabudu na kumtii Mungu. Wakati mwingine Mungu hutuma malaika "kuingiliana" kati kipindi cha ubinadamu. Utafiti wa malaika hutusaidia kutambua vita vinavyomo kati ya malaika wa Mungu na Shetani na pepo zake. Uelefu sahihi wa malaika ni muhimu sana. Tunapoelewa kwamba malaika ni viumbe, kama vile tulivyo, tunatambua kwamba kuabudu au kuomba kwa malaika kunamwibia Mungu utukufu ambao ni wake Yeye pekee. Alikuwa Mungu, si malaika, ambaye alimtuma Mwanawe afe kwa ajili yetu, ambaye anatupenda na kututunza, na ambaye peke yake anastahili kuabudiwa.

Mstari muhimu juu ya somo la malaika ni Waebrania 1:14, "Malaika ni nini ila roho wanaomtumikia Mungu na ambao hutumwa kuwasaidia wale watakaopokea wokovu?"

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, somo la malaika ni lini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries