settings icon
share icon
Swali

Hamatiolojia ni nini?

Jibu


Hamatiolojia ni utafiti wa dhambi. Hamatiolojia inahusika na jinsi dhambi ilivyotokana, jinsi inavyoathiri ubinadamu, na nini kitatokea baada ya kifo. Kwa dhambi kimsingi ina maana ya "kukosa alama." Sisi wote tunakosa alama ya Mungu ya haki (Warumi 3:23). Hamatiolojia, basi, inaelezea ni kwa nini tunakosa alama, jinsi tunakosa alama, na matokeo ya kukosa alama. Hizi ni baadhi ya maswali muhimu katika Hamatiolojia:

Ufafanuzi wa dhambi ni nini? Dhambi inaelezewa katika Biblia kama uvunjaji wa sheria ya Mungu (1 Yohana 3: 4) na uasi dhidi ya Mungu (Kumbukumbu la Torati 9: 7; Yoshua 1:18).

Je, sisi sote tulirithi dhambi kutoka kwa Adamu na Hawa? Warumi 5:12 inasema hivi, "Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi."

Je, dhambi zote ni sawa kwa Mungu? Kuna viwango vya dhambi — baadhi ya dhambi ni mbaya zaidi kuliko zengine. Wakati huo huo, kuhusiana na matokeo ya milele na wokovu, dhambi zote ni sawa. Kila dhambi husababisha hukumu ya milele (Warumi 6:23).

Ninawezaje kujua kama kitu ni dhambi? Kuna mambo ambayo Bibilia inatumbua na kusema kuwa ni dhambi. Suala ngumu zaidi ni katika kuamua dhambi ni nini katika hali ambazo Biblia haijazishughulikia moja kwa moja.

Inaweza kuonekana kuwa kusoma somo la kukandamiza kama dhambi ingekuwa kinyume na mazao kwa Mkristo. Baada ya yote, sisi hatujaokolewa kutoka kwa dhambi kwa damu ya Kristo? Ndiyo! Lakini kabla ya kuelewa wokovu, lazima kwanza tuelewe kwa nini tunahitaji wokovu. Hapoo ndipo Hamatiolojia inakuja. Inafafanua kwamba sisi wote ni wenye dhambi — kwa urithi, kwa kuambukiziwa, na kwa uchaguzi wetu wenyewe. Inatuonyesha kwa nini Mungu lazima atatuhukumu kwa ajili ya dhambi zetu. Hamatiolojia inaelezea suluhisho la dhambi — sadaka ya dhabihu ya Yesu Kristo. Wakati tunapokuja kukabiliana na asili zetu za dhambi, tunaanza kuelewa kina na ukubwa wa asili ya Mungu wetu mkuu ambaye, kwa upande mmoja, anawahukumu wafufu kuzimu kwa hukumu ya haki, basi, na kwa upande mwingine, hutimiza mahitaji Yake ya ukamilifu. Ni katika kuelewa pekee kina cha dhambi tunaweza kuelewa urefu wa upendo wa Mungu kwa wenye dhambi.

Andiko muhimu juu ya Hamatiolojia ni Warumi 3: 23-24, "kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu."

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Hamatiolojia ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries