settings icon
share icon
Swali

Muumini atahitajika kumiliki silaha?

Jibu


Kwa sababu ya idadi kubwa dhidi ya dhuluma duniani na kuzorota kwa umoja uliokuwemo katika maandishi,majadiliano ikiwa waumini wanaruhusiwa kumiliki silaha yangalipo.Ila katika maandiko yanatoa ufafanuzi kuhusu suala hili kutoka enzi za kale.

Katika maandiko kunao wafuasi waliomiliki silaha.Usiku ule alipotiwa mbaroni Yesu aliamuru wanafunzi wake kutoa silaha. Walimiliki mbili,na hapo Yesu akawahakikishia zilikuwa zatosha. (Luka 22: 37-39).Walipomshika Yesu, Petro alikata sikio la kiongozi mmoja kati ya wale waliomchukua. (Yohana 18:10).Mara hiyo Yesu alimponya bila kukawia (Luka 22:51) na kumshurutisha Petro aweke silaha mahali pake (Yohana 18:11). Petro kuwa na silaha haukuwa na madhara,ila jinsi aliyoitumia ndiyo ilikuwa na taabu.

Mara nyingine,wakuhani walijileta kupata ubatizo na kubatizwa naYohana Mbatizaji. Kuuliza wangetenda nini ili kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu,Yohana aliwajibu, "Mdhulumu mtu wala msishitaki kwa uongo;tena mtosheke na mshahara wenu " (Luka 3:14). Yohana hakuwadokezea kuacha kutumia silaha zao.

Kunaye Daudi, pia aliyemtukuza Mungu "anifundishaye mikono yangu vita,vidole vyangu kupigana" (Zaburi 144: 1). Agano la Kale hutoa mafundisho ya watu wa mungu waliokuwa na silaha na hata kuzitumia,ila tu wakati uliofaa katika vita.

Maandiko hayajamzuia muumini dhidi ya kuwa na silaha,ila hupeana mapendekezo kuhusiana nazo za kutiwa maanani. Mosi,muumini anafaa kuwa mlinda amani(Mathayo 5: 9).Muumini anafaa kutia maanani kuhusu umiliki wa silaha kama kuwa nayo utachangia kuweka Amani.

Pia, Muumini anafaa kufikiria ikiwa umiliki wa silaha utatukuza Mungu (1 Wakorintho 10:23). Matumizi ya silaha katika kuwinda,kufanikisha sharia, ama kujikinga kunadhaniwa kumtukuza Mungu. Ila mwanadamu anafaa kuwaza kuhusu malengo ya kuwa na silaha.

Tatu, Muumini anafaa kushika torati pamoja na kanuni zinazolinda sihala. Warumi 13 inafafanua ilivyo bora kwa mamlaka kuheshimiwa kwa maana hutoka kwa Mungu. Pamoja na hayo tunafaa kusali kwa sababu ya wakuu wetu wanaotoa mwongozo kwa nchi zetu. (1 Timotheo 2: 1-2).

Mwishowe hakuna dhambi yoyote katika kuwa na bunduki au silaha zozote. Silaha ina umuhimu na mara katika hali zingine;mara hiyo hiyo,waumini wanafaa kuchunguza malengo yao katika suala la kumiliki silaha ,hata kuzingatia kanuni zinazohusishwa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Muumini atahitajika kumiliki silaha?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries