settings icon
share icon
Swali

Je, Shetani yupo?

Jibu


Bibilia inatufahamisha wazi juu ya kuwepo kwa Shetani. Anaelezwa kama adui wa mwanadamu (Mwanzo 3:15), baba wa uongo (Yohana 8: 44b), na mshtakiwa (Ufunuo 12:10), na kati ya mambo mengine. Jina "Shetani" linamaanisha "adui." Isaya 14: 12-17 inaelezea kwamba apo mwanzo Shetani alikuwa malaika, lakini aliamua kwamba alitaka heshima na ibada kama ya Mungu tu na kutupwa kutoka mbinguni (pia angalia Ezekieli 28 : 11-17).

Kutoka wakati alitupwa kutoka mbinguni (pamoja na malaika waliochagua kuasi na yeye), Shetani amefanya kusudi lake la kupinga Mungu na kuwaongoza watu wa dunia kuwa waasi pia. Shetani ana mamlaka fulani katika ulimwengu huu; anaitwa "mungu wa wakati huu" (2 Wakorintho 4: 4) na "mkuu wa nguvu za hewa" (Waefeso 2: 2). Ndio sababu tunapaswa "mwe na kiasi na kukesha,kwa mshtaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye huzunguka-zunguka,akitafuta mtu ammeze "(1 Petro 5: 8).

Njia moja kubwa Shetani huharibu maisha yetu ni kwa udanganyifu.Wakati Shetani anatudanganya kuhusu Mungu ni nani, ambaye Mungu anasema tuko, na ni nani, yeye hupata nguvu na mamlaka katika maisha yetu. "Shetani hayupo" ni moja ya uongo mkubwa zaidi Shetani husema.

Katika uumbaji, Mungu aliwapa wanadamu mamlaka juu ya dunia (Mwanzo 1:28). Wakati Adamu na Hawa walipenda kutomtii Mungu, waliacha baadhi ya mamlaka yao; kwa kumsikiliza Shetani, walijipeana kwa shetani. Hata hivyo, msalabani, Yesu alimyanganya Shetani mamlaka yake: "Sasa ndio wakati wa hukumu juu ya ulimwengu huu; sasa mkuu wa ulimwengu huu atafukuzwa nje "(Yohana 12:31). "kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa ili azivunje kazi za Ibilisi " (1 Yohana 3: 8). Shetani hana mamlaka tena juu ya wale walio ndani ya Kristo, isipokuwa wanapompa hilo kwa kuamini uongo wake.

Taarifa nyingi za uongo kuhusu Shetani huja kutoka kwa maigizo na vyanzo vingine vya ujanja. Ni muhimu kwamba tunaenda kwa Bibilia kwa ukweli juu ya mambo haya na mengine. Bibilia inatuambia waziwazi kwamba Shetani yupo, na inatuambia jinsi anavyofanya. Hatuna sababu ya kutishiwa na Shetani, kwa kuwa nguvu zake ni duni sana kwa Mungu, lakini Bibilia inatufundisha kuwa tusiwe wazembe katika vita vya kiroho (Waefeso 6: 10-18). Kitu muhimu ni kujiwasilisha kwa Mungu na kumpinga shetani (Yakobo 4: 7), kujua kwamba Kristo amemshinda milele msalabani na hukumu ya mwisho ya Shetani-imehakikishwa (Ufunuo 19:20).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Shetani yupo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries