settings icon
share icon
Swali

Je! Shetani alikuwa nyoka anayetajwa katika Mwanzo sura ya 3?

Jibu


Ndiyo, nyoka katika Mwanzo sura ya 3 ilikuwa Shetani. Shetani alikuwa anaonekana kama nyoka, alimwingia nyoka, au kumdanganya Adamu na Hawa kuamini kwamba alikuwa nyoka ambaye alikuwa akizungumza nao. Nyoka hazina uwezo wa kuzungumza. Ufunuo 12: 9 na 20: 2 inaelezea Shetani kama nyoka. " Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu.'' (Ufunuo 20: 2). " Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye." (Ufunuo 12: 9).

Haijawekwa wazi katika Biblia ya kwamba nyoka alisimama kabla ya laana, au alitembea kabla ya laana. Inaonekana na inawezekana kwamba, kama vile viumbe wengine, huenda alitembea kwa miguu minne. Hiyo inaonekana kuwa ni ufafanuzi bora zaidi wa Mwanzo 3:14, " Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako.'' Ukweli kwamba nyoka ililaaniwa kutambaa kwa tumbo lake na kula udongo wa dunia milele pia ni njia ya kuonyesha kwamba nyoka ingekuwa ya kuchukiwa milele na kuonekana kama kiumbe kibaya na cha kudharauliwa.

Kwa nini Mungu alilaani nyoka na alijua kwamba ni Shetani ambaye alikuwa amesababisha Adamu na Hawa kufanya dhambi? Hatima ya nyoka ni mfano. Laana ya nyoka siku moja itakuwa hatima ya Shetani mwenyewe (Ufunuo 20:10; Ezekieli 28: 18-19).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Shetani alikuwa nyoka anayetajwa katika Mwanzo sura ya 3?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries