settings icon
share icon
Swali

Ni nini kusudi la Sheria ya Musa?

Jibu


Sheria ya Musa ilitolewa hasa kwa taifa la Israeli (Kutoka 19; Mambo ya Walawi 26:46; Warumi 9: 4). Ilikuwa na sehemu tatu: Amri Kumi, maagizo, na mfumo wa ibada, ambao ulihusisha ukuhani, hema, sadaka, na sherehe (Kutoka 20-40; Mambo ya Walawi 1-7; 23). Kusudi la Sheria ya Musa ilikuwa ukamilisha zifuatazo:

(1) Kufunua tabia takatifu ya Mungu wa milele kwa taifa la Israeli (Mambo ya Walawi 19: 2; 20: 7-8).

(2) Kutia wakifu taifa la Israeli kuwa tofauti na mataifa mengine yote (Kutoka 19: 5).

(3) Kufunua asili ya dhambi ya mwanadamu (tazama Wagalatia 3:19). Ingawa Sheria ilikuwa nzuri na takatifu (Warumi 7:12), haikutoa wokovu kwa taifa la Israeli. "kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria" (Waroma 3:20; tazama Matendo 13: 38-39).

(4) Kutoa msamaha kupitia dhabihu / sadaka (Mambo ya Walawi 1-7) kwa watu ambao walikuwa na imani katika Bwana katika taifa la Israeli.

(5) Kutoa mwongozo wa ibada kwa jamii ya imani kupitia sikukuu za kila mwaka (Mambo ya Walawi 23).

(6) Kutoa mwongozo wa Mungu kwa afya ya kimwili na kiroho ya taifa (Kutoka 21-23, Kumbukumbu la Torati 6: 4-19; Zaburi 119: 97-104).

(7) Kuwasababisha watu, baada ya Kristo kuja, kuona kwamba hawakuweza kuzingatia Sheria lakini walihitaji kumkubali Kristo kama Mwokozi wao kibinafsi, kwa kuwa Ametimiza Sheria katika maisha yake na kulipa adhabu ya dhambi zetu katika kifo chake, kuzikwa, na ufufuo wa kimwili (Wagalatia 3:24; Warumi 10: 4). Muumini katika Kristo ana haki sawa na ile ya Sheria iliyotimizwa ndani yake ikiwa atatii Roho Mtakatifu anayeishi ndani yake (Warumi 8: 4).

Kusudi la Torati ya Musa linafufua maswali haya: "Je, unajiamini wewe mwenyewe kuitunza Sheria yote wakati wote (ambayo huwezi kufanya)?" Au "Je, umefanya uchaguzi kumkubali Yesu kama Mwokozi wako, akijua kwamba Yeye amekamilisha Sheria yote kabisa, hata kulipa adhabu yako kwa kuivunja? "Chaguo ni lako.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni nini kusudi la Sheria ya Musa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries