settings icon
share icon
Swali

Je! Biblia inatabiri serikali moja ya ulimwengu na sarafu moja ya ulimwengu katika nyakati za mwisho?

Jibu


Biblia haitumii maneno "serikali moja ya ulimwengu" au "sarafu moja ya ulimwengu" kwa kutaja nyakati za mwisho. Inafanya, hata hivyo, kutoa ushahidi wa kutosha ili kutuwezesha kufikia hitimisho kwamba yote yatakuepo chini ya utawala wa Mpinga Kristo katika siku za mwisho.

Katika maono yake ya kiyama katika kitabu cha Ufunuo, mtume Yohana anaona "Mnyama," anayeitwa pia Mpinga Kristo, akiinuka kutoka baharini. Mnyama huyu ana vichwa saba na pembe kumi (Ufunuo 13:1). Kuchanganya maono haya sawa na ya Danieli (Danieli 7:16-24), tunaweza kuhitimisha kwamba aina fulani ya mfumo wa kisiasa duniani utazinduliwa na mnyama, "pembe" yenye nguvu zaidi, ambaye atashinda wafalme watatu kati ya kumi na kuendeleza vita dhidi ya Wakristo. Shirikisho la mataifa kumi linaonekana pia katika sura ya Danieli ya sanamu katika Danieli 2:41-42. Katika maono haya serikali ya mwisho ya dunia iliyo na vyombo kumi inawakilishwa na vidole kumi vya sanamu. Yeyote ambaye ni kumi na hata hivyo wanaingia kwa utawala, Maandiko ni wazi kwamba mnyama atainuka kwa utawala kutoka katikati mwao na kuwa mfalme maarufu zaidi kati yao. Mwishoni, wafalme wengine watafanya amri zake.

Yohana anaelezea mtawala wa ufalme huu mkubwa kama mwenye nguvu na mamlaka kuu, aliyopewa na Shetani mwenyewe (Ufunuo 13:2). Anapokea ibada kutoka "ulimwengu mzima" (13:3-4) na ana mamlaka juu ya "kila kabila na jamaa na lugha na taifa" (13:7). Kutoka kwa maelezo haya, ni mantiki kusadiki kwamba mtu huyu ni kiongozi wa serikali moja ya ulimwengu ambayo inajulikana kuwa huru juu ya serikali zingine zote. Ni vigumu kufikiria jinsi serikali hizo mbalimbali vile ziko mamlakani leo zinaweza kujitiisha zenyewe kwa mtawala mmoja, na kuna nadharia nyingi juu ya suala. Dhana moja ni kwamba maafa na tauni yaliyotajwa katika Ufunuo kama hukumu za muhuri na tarumbeta (sura ya 6-11) zitakuwa mbaya sana na kuunda mgogoro mkubwa sana wa ulimwengu ambao watu watakubaliana na mtu yeyote anayeahidi msaada.

Mara baada ya kuingia kwa utawala, mnyama (Mpinga Kristo) na nguvu nyuma yake (Shetani) atahamia kuanzisha udhibiti kamili juu ya watu wote wa dunia. Mwisho wao wa kweli ni kupokea ibada Shetani amekuwa akitafuta tangu kutupwa kutoka mbinguni (Isaya 14:12-14). Njia moja watakayotimiza hii ni kwa kudhibiti biashara zote, ambapo wazo la sarafu moja ya ulimwengu inakujia. Ufunuo 13:16-17 inaelezea aina fulani ya alama ya kishetani ambayo itahitajika ili kununua na kuuza. Mtu yeyote anayekataa alama atashindwa kununua chakula, mavazi, au mahitaji mengine ya kimsingi. Bila shaka idadi kubwa ya watu duniani watapata alama ili waishi. Mstari wa 16 hufafanua kwamba hii itakuwa mfumo wa ulimwengu wote ambao kila mtu, matajiri na maskini, mkuu na mdogo, watachukua alama kwenye mkono au paji la uso wao. Kuna uvumi mwingi kuhusu jinsi alama hii itawekwa, lakini teknolojia zinazopatikana sasa hivi zinaweza kukamilisha kwa urahisi sana.

Wale watakaoachwa nyuma baada ya kunyakuliwa kwa Kanisa watakuwa wanakabiliwa na uchaguzi kali sana-kubali alama ya mnyama ili kuishi au kabiliana na njaa na mateso mabaya na Mpinga Kristo na wafuasi wake. Lakini wale wataokuja kwa Kristo wakati huu, wale ambao majina yao yameandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo (Ufunuo 13:8), watachagua kuvumilia, hata mateso/kifo cha kishahidi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Biblia inatabiri serikali moja ya ulimwengu na sarafu moja ya ulimwengu katika nyakati za mwisho?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries