settings icon
share icon
Swali

Je! siku ya Sabato ni nini?

Jibu


Kwa mtazamo wa kwanza, swali "Ni nini maana ya siku ya Sabato?" inaonekana rahisi sana. Kulingana na Kutoka 20: 8–11, Sabato ni siku ya saba ya juma, ambayo tunapaswa kupumzika, kwa kukumbuka kwamba Mungu aliumba ulimwengu kwa siku sita na kisha "akapumzika" siku ya saba. Walakini, kwa sababu ya kutokuelewa na kutafsiri vibaya kwa baadhi ya vikundi vya Kikristo, maana ya mapumziko ya siku ya Sabato imeeleweka vibaya.

Baadhi ya vikundi vya Kikristo, kama vile Wasabato, wanaiona Sabato kama siku ya ibada, siku ambayo Wakristo wanapaswa kuhudhuria ibada ya kanisa / ibada. Huku vikundi hivi kwa kawaida vikifundisha kwamba hakuna kazi inayostahili kufanywa siku ya Sabato, dhana ya "siku ya kuabudu" wakati mwingine wanasisitiza kuwa ni "siku ya kupumzika." Hapo mbeleni, Sabato ilikuwa siku ya mapumziko, na kusudi hilo lilihifadhiwa katika Sheria ya Musa (Kutoka 16: 23–29; 31: 14-16; 35: 2-3; Kumbukumbu la Torati 5: 12-15; Nehemia 13:15 -22; Yeremia 17: 21-27). Katika Agano la Kale, dhabihu zilitolewa kila siku kwenye madhabahu / hekalu. "Ibada" ilikuwa ya kila wakati. Na kulikuwa na maagizo maalum yaliyopewa Israeli kuhusu "mkusanyiko takatifu" uliofanyika siku ya Sabato (Walawi 23: 3; vile vile Hesabu 28: 9). Utunzaji wa Sabato ulikuwa "ishara" ya agano kati ya Israeli na Bwana (Kutoka 31:13).

Agano Jipya limenakili Wayahudi na waongofu kwa Wayahudi wakikutana katika masinagogi siku ya Sabato (Marko 6: 2; Luka 4:31; Luka 13: 10-16; Matendo 13:14, 27, 42–44; 15:21; 13; 17: 2; 18: 4). Kwa wazi, bila kufanya kazi yoyote siku ya Sabato, siku ya Sabato ingekuwa siku nzuri ya kuwa na ibada. Walakini, Agano Jipya haliamuru kwamba Sabato iwe siku ya ibada. Kanisa haliko chini ya Sheria ya Musa.

Kanisa liko chini ya Agano Jipya, lilianzishwa kwa misingi ya kifo na kufufuka kwa Yesu Kristo. Hamna mahali Biblia inaelezea kwamba Wakristo walitenga siku ya Sabato kama siku yao ya kuabudu. Maandiko pekee yanayoelezea Wakristo kukutana siku ya Sabato kwa hakika yanalenga kazi ya uinjilisti katika masinagogi ya Kiyahudi ambao walikutana siku ya Sabato. Matendo 2:46 imenakili kwamba Wakristo wa kwanza walikutana kila siku. Waberoya waliyachunguza Maandiko kila siku (Matendo 17:11). Matendo 20:7 na 1 Wakorintho 16:2 zote zinawataja Wakristo kukutana siku ya kwanza ya juma. Hamna Ushahidi wowote katika Agano Jipya wa kuwa mitume au Wakristo wa kwanza katika hali yoyote waliadhimisha siku ya Sabato kama siku ya ibada.

Tangu jadi, Wakristo wamefanya ibada zao za kimsingi siku ya Jumapili, siku ya kwanza ya juma, katika kusherehekea ufufuo wa Kristo, ambao ulitokea Jumapili (Mathayo 28: 1; Marko 16: 2; Luka 24: 1; Yohana 20: 1). Ni muhimu kuelewa, hata hivyo, kwamba Jumapili sio siku iliyoamriwa ya ibada ya ushirika, pia. Hakuna amri dhahiri ya kibiblia kwamba Jumamosi au Jumapili iwe siku ya ibada. Maandiko kama Warumi 14: 5-6 na Wakolosai 2:16 huwapa Wakristo uhuru wa kuadhimisha siku maalum au kuzingatia kila siku kuwa maalum. Kusudi la Mungu ni kuwa tumwabudu na kumtumikia Yeye daima, kila siku, sio tu Jumamosi au Jumapili pekee.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! siku ya Sabato ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries