settings icon
share icon
Swali

Je, preterist wa sehemu wanaamini nini? Je, preterism ya sehemu ni ya kibiblia?

Jibu


Preterism ni mtazamo wa kitheolojia inayoshughulika na kifo, hukumu, pepo na jahanamu kwamba unabii wa "nyakati za mwisho" wa Biblia umetimizwa tayari. Kwa hivyo, tunaposoma kile Biblia inasema kuhusu dhiki, tunasoma historia. Preterism imegawanywa katika kambi mbili: preterism kamili (au thabiti) na preterism ya sehemu. Preterism kamili imechukua mawazo yasiyo na kadiri kwamba unabii wote katika Biblia umetimizwa kwa njia moja au nyingine. Preterists wa sehemu huchukua mbinu ya wastani zaidi, na wengi wa preterists wa sehemu wanafikiri kuwa preterists kamili kuwa na hatia ya uasi.

Wale ambao wanashikilia preterism ya sehemu wanaamini kuwa unabii katika Danieli, Mathayo 24, na Ufunuo (isipokuwa ya sura mbili au tatu za mwisho) tayari umetimizwa na ulitimizwa kabla ya karne ya kwanza baada Kristo. Kulingana na preterism ya sehemu, hakuna unyakuo, na vifungu vinavyoelezea dhiki na Mpinga Kristo hasa vinarejelea uharibifu wa Yerusalemu katika 70 Baada ya Kristo na mfalme wa Kirumi Tito. Preterists wa sehemu wanaamini kurudi kwa Kristo duniani na ufufuo na hukumu wa baadaye, lakini hawafundishi ufalme wa milenia au kwamba Israeli kama taifa ina nafasi katika mpango wa Mungu wa baadaye. Kulingana na preterists wa sehemu, maandiko ya Biblia ya "siku za mwisho" yanasema juu ya siku za mwisho za Agano la Kale la Kiyahudi, si siku za mwisho za dunia yenyewe.

Kwa kuwa preterists wa sehemu kudumisha msimamo wao, wanasisitiza kuwa kitabu cha Ufunuo kiliandikwa mapema (kabla ya 70 Baada ya Kristo). Wanapaswa pia kutumia mbinu isiothabiti wakati wa kutafsiri vifungu vya unabii. Kulingana na mtazamo wa preterist wa nyakati za mwisho, sura ya 6-18 ya Ufunuo ni ya mfano wa juu, si kuelezea matukio yoyote halisi. Tangu uharibifu wa Yerusalemu haukuhusisha uharibifu wa jumla wa maisha ya bahari (Ufunuo 16:3) au giza kali (mstari wa 10), hukumu hizi zinatafsiriwa na preterist kama kiistiari. Hata hivyo, kulingana na preterists, sura ya 19 inapaswa kueleweka halisi-Yesu Kristo atarudi kimwili. Lakini sura ya 20 imetafsiriwa tena kiistiari na preterists, wakati huo huo sura ya 21-22 zinaeleweka halisi, angalau kwa sehemu, kwa kuwa kuna kweli mbingu mpya na dunia mpya.

Hakuna mtu anakataa kwamba Ufunuo ina maono ya kushangaza na wakati mwingine ya kuchanganya. Hakuna mtu anayekana kwamba Ufunuo inaelezea vitu vingi kitamathali-hiyo ni asili ya fasihi ya kiyama. Hata hivyo, kwa hakika kukataa asili halisi ya sehemu ya vipengele vya Ufunuo ni kuharibu msingi wa kutafsiri kitabu chochote kihalisi. Ikiwa mateso, mashahidi, mnyama, nabii wa uongo, ufalme wa milenia, nk, yote ni kiistiari, basi ni kwa msingi gani tunadai kwamba kuja kwa mara ya pili wa Kristo na dunia mpya ni halisi? Hiyo ni kushindwa kwa preterism-inachaacha tafsiri ya Ufunuo kwa maoni ya mkalimani.

Wale wanaoshikilia preterism ya sehemu pia hawasomi Mathayo 24 kwa maana halisi. Kristo alizungumza kuhusu uharibifu wa hekalu (Mathayo 24:2). Lakini mengi ya yale aliyoyaelezea hayakutokea katika AD 70. Kristo anazungumzia wakati huo ujao kama moja wa "dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu yeyote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo" (Mathayo 24:21-22). Hakika, hii haiwezi kutumika kwa matukio ya AD 70. Kumekuwa na nyakati mbaya zaidi katika historia ya dunia tangu wakati huo

Bwana pia anasema, "Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika; ndipo itakapoonekena ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi"(Mathayo 24:29-30). Kwa kuwa matukio ya aya hizi mbili tayari yametokea, Yesu Kristo lazima alirejea kimwili katika 70 Baada ya Kristo-lakini hakurudi. Preterist wa sehemu anaamini kwamba aya hizi hazitaji kurudi wa kimwili wa Kristo bali kuonekana kwa hukumu Yake. Hata hivyo, hii sio kawaida, kusoma halisi wa maandishi itasababisha mtu yeyote kuamini. Ni "Mwana wa Adamu" ambaye watu wanaona, si tu hukumu Yake.

Preterists wa sehemu pia wanakata rufaa kwenye Mathayo 24:34 ambapo Yesu anasema juu ya "kizazi hiki." Wanasema Kristo alikuwa akimaanisha wale waliokuwa wakiishi wakati aliongea maneno yaliyoandikwa katika sura hiyo; hivyo, dhiki inapaswa kutokea ndani ya miaka 40 ya maneno Yake. Hata hivyo, tunaamini kuwa Yesu hakuwa akizungumzia watu wa siku Yake bali kwa kizazi ambacho kitashuhudia matukio yaliyoandikwa katika Mathayo 24:15-31. Kizazi hicho cha baadaye kitashuhudia matukio yote ya kusonga kwa haraka ya siku za mwisho, ikiwa ni pamoja na kurudi kimwili wa Kristo (mistari 29-30).

Mtazamo wa preterist wa sehemu unasababisha imani katika umilenia (au baada ya umilenia) na inahusishwa na teolojia ya agano. Bila shaka, inakataa ugawaji. Lakini shida yake kuu ni mbinu yake isiyothabiti na istiari yake ya unabii mwingi wa kibiblia ambao unaeleweka halisi. Wakati huo huo preterism ya sehemu ni ndani ya wigo wa kidini, sio maoni mengi kati ya Wakristo leo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, preterist wa sehemu wanaamini nini? Je, preterism ya sehemu ni ya kibiblia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries