settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kuwa na nia ya Kristo?

Jibu


Katika 1 Wakorintho 2:16, Paulo anukuu Isaya 40:13 na kisha anatoa taarifa juu ya waumini wote: "Tunayo nia ya Kristo." Kuwa na nia ya Kristo kunamaanisha kushiriki mpango, kusudi, na mtazamo wa Kristo, na ni kitu ambacho waumini wote wako nayo.

Kuwa na nia ya Kristo inamaanisha sisi kuelewa mpango wa Mungu duniani — kuleta utukufu Kwakwe, kurejesha uumbaji kwa utukufu wake wa awali, na kutoa wokovu kwa wenye dhambi. Ina maana kuwa sisi tunajitambulisha na kusudi la Kristo "kutafuta na kuokoa kile kilichopotea" (Luka 19:10). Ina maana tunashiriki mtazamo wa Yesu wa unyenyekevu na utii (Wafilipi 2: 5-8), huruma (Mathayo 9:36), na katika maombi kumtegemea Mungu (Luka 5:16).

Katika mistari inayotuongoza kwa 1 Wakorintho 2:16, tunaona ukweli fulani kuhusu nia ya Kristo:

1) Nia ya Kristo inatofautiana sana na hekima ya mwanadamu (mistari 5-6).

2) Nia ya Kristo inahusisha hekima kutoka kwa Mungu, ambayo wakati moja ilikuwa lakini sasa imefunuliwa (mstari wa 7).

3) Nia ya Kristo imetolewa kwa waumini kupitia Roho wa Mungu (mistari 10-12).

4) Nia ya Kristo haiwezi kueleweka kwa wale wasio na Roho (mstari wa 14).

5) Nia ya Kristo inawapa waumini ufahamu katika mambo ya kiroho (mstari wa 15).

Ili kuwa na nia ya Kristo, mtu lazima awe na imani ya kwanza katika Kristo (Yohana 1:12, 1 Yohana 5:12). Baada ya wokovu, muumini anaishi maisha chini ya ushawishi wa Mungu. Roho Mtakatifu anakaa na kumpa muumini mwangaza, akimwingiza kwa hekima-akili ya Kristo. Waumini wako na wajibu wa kujitoa kwa uongozi wa Roho (Waefeso 4:30) na kuruhusu Roho kubadilisha na kupanua mawazo yake (Warumi 12: 1-2).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kuwa na nia ya Kristo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries