settings icon
share icon
Swali

Ngono kabla ya ndoa — kwa nini Wakristo wanaipingavikali sana?

Jibu


Ngono kabla ya ndoa inahusisha aina yoyote ya ngono kabla ya kuingia katika uhusiano wa ndoa ya kisheria. Kuna sababu kadhaa ambazo Maandiko na Ukristo wa jadi hupinga hii. Mungu alifanya ngono ili kufurahiwa ndani ya uhusiano wa ndoa uliofanywa na mwanaume mmoja na mwanamke mmoja. Ili kuiondoa kwenye hali hiyo ni kupotosha matumizi yake na kupunguza kikamilifu radhi yake. Mawasiliano ya ngono inahusisha kiwango cha urafiki usio na uzoefu katika uhusiano wowote mwingine wa binadamu. Wakati Mungu alileta Adamu na Hawa katika ndoa, alianzisha uhusiano wa "mwili mmoja". Mwanzo 2:24 inatuambia kwamba mwanaume ataacha familia yake, kujiunga na mkewe, na kuwa "mwili mmoja" pamoja naye.

Dhana hii inafanywa kupitia katika Agano Jipya pia; tunaiona katika maneno ya Yesu katika Mathayo 19:5 na Marko 10:7. Paulo anaeleza juu ya wazo katika 1 Wakorintho 6:12-20, katika majadiliano yake juu ya utawala wa Mungu juu ya miili yetu na nafsi zetu. Anasema kwamba wakati mtu anafanya ngono na kahaba, wamekuwa "mwili mmoja" (mstari wa 16). Ni wazi kwamba uhusiano wa ngono ni maalum. Kuna ngazi ya hatari ya mtu upitia katika uhusiano wa ngono ambao unapaswa kutokea tu ndani ya muungano wa ndoa uliojitolea, uaminifu.

Kuna, kwa ujumla, mazingira mawili ya ngono kabla ya ndoa. Kuna "tunapendana na tunajitolea kwa kila mmoja, lakini hatutaki kusubiri kuoana" uhusiano wa ngono, na kuna "ngono ya kawaida." Ya kwanza mara nyingi hutazamwa kimantiki na wazo kwamba wanandoa hakika wataoana, hivyo hakuna dhambi katika kushiriki katika mahusiano ya kabla ndoa sasa. Hata hivyo, hii inaonyesha kutokuwa na uvumilivu na kutojiheshimu mwenyewe, vile vile kwa mtu mwingine. Inachukua asili maalum ya uhusiano kutoka kwa mfumo wake sahihi, ambayo itafuta wazo kwamba kuna mfumo kabisa. Ikiwa tunakubali tabia hii, si muda mrefu kabla tukubali ngono yoyote nje ya ndoa kama inakubalika. Ili kuwaambia waenzi wetu kwamba wanastahili kuwa na subirá kwa kuimarisha uhusiano na kuongeza kiwango cha kujitolea.

Ngono ya kawaida imeenea sana katika jamii nyingi. Kuna, kwa hakika, hakuna kitu kama ngono ya "kawaida", kwa sababu ya kina cha urafiki unaohusika katika uhusiano wa ngono. Analojia ni mafundisho hapa. Ikiwa tukinatisha kitu kimoja kwa kingine, kitanata. Ikiwa tutakiondoa, itaacha nyuma kiasi kidogo cha mabaki; ikibaki kwa muda, mabaki zaidi ya yanaachwa. Ikiwa tutachukua kitu hicho kilichonatwa na kukiweka kwenye maeneo kadhaa mara kwa mara, itaacha mabaki kila mahali tunatisha, na hatimaye itapoteza uwezo wake wa kuambatana na chochote. Hii ni kama vile kinachotokea kwetu tunaposhiriki ngono "ya kawaida". Kila wakati tunatoka uhusiano wa ngono, tunaacha sehemu yetu wenyewe nyuma. Uhusiano huo ukiendelea kwa muda, zaidi tunaacha nyuma, na zaidi tunapoteza wenyewe. Tunapoenda kutoka kwa mpenzi hadi mpenzi, tunaendelea kupoteza sehemu kidogo yetu wenyewe kila wakati, na hatimaye tunaweza kupoteza uwezo wetu wa kuunda uhusiano wa ngono kudumu kabisa. Uhusiano wa kingono ni wenye nguvu sana na huwa karibu sana kwamba hatuwezi kuingia ndani yake kawaida, bila kujali ni jinsi gani inaweza kuonekana rahisi.

Hivyo, kuna tumaini? Wakati Mkristo anaposhiriki ngono kabla ya ndoa, au wakati mtu aliyepoteza ubikira/umwanamwali wake kuja kwa Kristo, Roho Mtakatifu atahukumu dhambi hiyo, na kutakuwa na huzuni juu yake. Hata hivyo, ni muhimu-hata muhimu zaidi-kukumbuka kwamba hakuna dhambi zaidi ya kufikiwa na damu ya Yesu. Ikiwa tutakiri, hatatusamehe tu, bali atatutakasa kutoka "uovu wote" (1 Yohana 1:9). Zaidi ya hayo, pamoja na msamaha (ambayo ni katika utukufu yenyewe), Mungu hurejesha. Katika Yoeli 2:25 Mungu anamwambia Israeli kwamba angeweza kurejesha miaka ambayo nzige zilikula. Hii si ahadi moja kwa moja kwa Wakristo leo, lakini inaonyesha kwamba Mungu ana tabia ya kurejesha. Ngono kabla ya ndoa ni kama nzige ambayo uharibu maana yetu wenyewe, kujistahi, na mtazamo wetu wa msamaha. Lakini Mungu anaweza kurejesha mambo hayo yote. Maandiko pia yanatuambia kwamba, tunapokuja kwa Kristo, sisi ni uumbaji mpya (2 Wakorintho 5:17), hivyo mtu aliyefanya ngono kabla ya kuolewa kabla ya uongofu uumbwa na Mungu kuwa mtu mpya; wa zamani ameenda, mpya imekuja.

Hatimaye, tunajua kwamba, kama Wakristo, tunafanywa upya na Roho Mtakatifu kila siku tunatembea pamoja na Yesu. Wakolosai 3:10 inatuambia kwamba nafsi yetu inaendelea kufanywa upya siku kwa siku baada ya sura ya Muumba wake. Hakuna dhambi bila tumaini. Nguvu ya injili inapatikana kwa wote wanaomwamini Yesu kwa msamaha.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ngono kabla ya ndoa — kwa nini Wakristo wanaipingavikali sana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries