settings icon
share icon
Swali

Je, ni nani atakayeenda mbinguni?

Jibu


Watu wana mawazo tofauti kuhusu mbinguni. Wengi hawana ufahamu wa Mungu hata kidogo, lakini bado wanapenda kufikiria mbinguni kuwa "mahali pazuri" ambako sisi sote huenda tunapokufa. Mawazo juu ya mbinguni mara nyingi si zaidi ya matumaini yasiyo wazi, na kuambatana na "labda nitashinda bahati nasibu siku fulani." Watu wengi hawafikirii mbinguni kwa makini hadi wanapohudhuria mazishi au wapendwa wao wanapokufa. Ni maarufu kutaja mbinguni kama mahali ambapo "watu wema huenda." Na bila shaka, kila mtu wanayejua na kupenda ako katika kikundi cha "watu wema."

Lakini Biblia ina mengi ya kusema juu ya uzima baada ya kifo, na inapingana na maoni maarufu. Yohana 3:16 inasema, " Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele." Kisha katika mstari wa 36, Yesu anaendelea kusema, " Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.Waebrania 9:27 inasema, " Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu." Kwa mujibu wa aya hizi, kila mtu hufa, lakini si kila mtu anayeenda mbinguni (Mathayo 25:46, Warumi 6:23; Luka 12: 5; Marko 9:43).

Mungu ni mtakatifu na mkamilifu. Mbinguni, makao yake, ni takatifu na kamilifu, pia (Zaburi 68: 5; Nehemia 1: 5; Ufunuo 11:19). Kulingana na Warumi 3:10, "hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja." Hakuna mwanadamu aliye mtakatifu na kamilifu kwa ajili ya mbinguni. Watu tunaowaita "wema" sio wema kabisa ikilinganishwa na ukamilifu usio na dhambi wa Mungu. Ikiwa Mungu angeruhusu wanadamu wenye dhambi kuingia ukamilifu wa mbinguni, haingekuwa tena kamilifu. Ni kiwango gani kinachopaswa kutumiwa kuamua ni nani "mwema wa kutosha?" Kiwango cha Mungu ni cha pekee ambacho kinahesabiwa, na Yeye tayari ametawala. Warumi 3:23 inasema kwamba "wote wamefanya dhambi na wamepungukiwa na utukufu wa Mungu." Na malipo ya dhambi hiyo ni kutengwa milele na Mungu (Warumi 6:23).

Dhambi inapaswa kuadhibiwa, au Mungu sio wa haki (2 Wathesalonike 1: 6). Hukumu tunayopata wakati wa kifo ni Mungu tu huweka rekodi zetu kuwa sahihi na kutupatia hukumu juu ya makosa yetu dhidi yake. Hatuna njia ya kufanya makosa yetu kuwa sawa. Uzuri wetu hauzidi ubaya wetu. Dhambi moja huharibu ukamilifu, kama vile tone moja la arsenic katika glesi ya maji hutia sumu glesi mzima.

Kwa hivyo Mungu akawa mtu na akachukua adhabu yetu juu yake. Yesu alikuwa Mungu katika mwili. Aliishi maisha yasiyo na dhambi ya utiifu kwa Baba Yake (Waebrania 4:15). Hakuwa na dhambi, lakini msalabani alichukua dhambi zetu na akazifanya kuwa zake. Mara alipolipia bei ya dhambi zetu, tunaweza kutangazwa kuwa takatifu na kamilifu (2 Wakorintho 5:21). Tunapokiri dhambi zetu kwake na kumwomba msamaha wake, Yeye hupiga muhuri "imelipwa kwa ukamilifu" juu ya maisha yetu ya ubinafsi, tamaa ya wanawake, na tamaa ya mali (Matendo 2:38, 3:19, 1 Petro 3:18).

Tunaposimama mbele ya Mungu siku moja, hatuwezi kuomba kuingia mbinguni kulingana na sifa zetu wenyewe. Hatuna chochote cha kutoa. Ikilinganishwa na kiwango cha Mungu cha utakatifu, hakuna hata mmoja wetu mwema. Lakini Yesu ni mwema, na ni kwa sifa yake tunaweza kuingia mbinguni. Wakorintho wa kwanza 6: 9-11 inasema, " Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi. Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu. " Sadaka ya Yesu inafunika yote.

Watu ambao wanaoenda mbinguni wote ni sawa kwa njia moja: wao ni wenye dhambi ambao wameweka imani yao katika Bwana Yesu Kristo (Yohana 1:12; Matendo 16:31; Waroma 10: 9). Wamegundua haja yao ya Mwokozi na kukubali kwa unyenyekevu utoaji wa msamaha wa Mungu. Wamekiri njia zao za zamani za kuishi na kuweka mtazamo wao kumfuata Kristo (Marko 8:34; Yohana 15:14). Hawajaribu kupata msamaha wa Mungu lakini wamemtumikia kwa furaha kutokana na mioyo ya kushukuru (Zaburi 100: 2). Aina ya imani inayookoa nafsi ni moja ambayo hubadilisha maisha (Yakobo 2:26; 1 Yohana 3: 9-10) na hutegemea kikamilifu neema ya Mungu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni nani atakayeenda mbinguni?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries