settings icon
share icon
Swali

Nani nabii wa uongo wa nyakati za mwisho?

Jibu


Nabii wa uongo wa nyakati za mwisho ameelezwa katika Ufunuo 13: 11-15. Yeye pia hujulikana kama "mnyama wa pili" (Ufunuo 16:13, 19:20, 20:10). Pamoja na Mpinga Kristo na Shetani, ambaye anawapa nguvu wote wawili, nabii wa uongo ni chama cha tatu katika utatu wa uongo.

Mtume Yohana anaelezea mtu huyu na anatupa dalili za kumtambua wakati anajitokesha. Kwanza, anatoka duniani. Hii inaweza kumaanisha kwamba anakuja kutoka shimo la kuzimu na nguvu zote za pepo za Jahannamu kwa amri yake. Inaweza pia kumaanisha kwamba anatoka kwa hali ya chini, siri na haijulikani hadi atakapopasuka kwenye jukwaa la ulimwengu kwenye mkono wa kulia wa Mpinga Kristo. Anaonyeshwa kama ana pembe kama mwana-kondoo, akizungumza kama zimwi. Pembe kwa mwana kondoo ni uvimbe tu juu ya vichwa vyao mpaka mwana kondoo atakua kondoo dume. Badala ya kuwa na uongezeko wa Mpinga Kristo wa vichwa na pembe, akionyesha uwezo wake na nguvu na ukali, nabii wa uongo huja kama mwana-kondoo, kwa kupendeza, na maneno ya kushawishi ambayo yanabembeleza kuwa na huruma na mapenzi mema kutoka kwa wengine. Anaweza kuwa mhubiri wa ajabu au msemi ambaye maneno yenye nguvu za kiushetani huwadanganya watu. Lakini anaongea kama zimwi, maana yake ujumbe wake ni ujumbe wa zimwi. Ufunuo 12: 9 hubainisha zimwi kama ibilisi na Shetani.

Mstari wa 12 inatupa ujumbe wa nabii wa uongo duniani, ambao ni kulazimisha wanadamu kumwabudu Mpinga Kristo. Ana mamlaka yote ya Mpinga Kristo kwa sababu, kama yeye, nabii wa uongo anapewa nguvu na Shetani. Haieleweki kama watu wanalazimika kuabudu Mpinga Kristo au kama wanapendezwa sana na viumbe hawa wenye nguvu kwamba wanaanguka kwa udanganyifu na kumwabudu kwa hiari. Ukweli kwamba mnyama wa pili anatumia ishara za miujiza na maajabu, ikiwa ni pamoja na moto kutoka mbinguni, ili kuhakikisha uaminifu wa wote wawili utaonekana kuonyesha kwamba watu wataanguka mbele yao katika ibada ya nguvu na ujumbe wao. Mstari wa 14 unaendelea kusema udanganyifu utakuwa mkubwa kiasi kwamba watu wataanzisha sanamu kwa Mpinga Kristo na kuabudu. Hii ni kukumbusha sanamu kubwa ya dhahabu ya Nebukadneza (Danieli 3) ambayo wote wangepaswa kuinama mbele yake na kuiheshimu. Ufunuo 14: 9-11, hata hivyo, inaelezea athari mbaya ambayo inasubiri wale wanaoabudu sanamu ya Mpinga Kristo.

Wale ambao wanaokoka hofu ya Dhiki kwa hatua hii watakuwa wanakabiliwa na uchaguzi mbili ngumu. Wale wanaokataa kuabudu sanamu ya mnyama watakuwa chini ya kifo (mstari wa 15), lakini wale wanaomwabudu yeye watapata ghadhabu ya Mungu. Sanamu hiyo itakuwa ya ajabu kwa kuwa itaweza "kuzungumza." Hii haimaanishi kuwa itakuja uzima — neno la Kiyunani hapa ni pneuma linamaanisha "pumzi" au "mkondo" wa hewa, si neno bios (" maisha ") — lakini ina maana kwamba itakuwa na aina fulani ya uwezo wa kupumua ujumbe wa Mpinga Kristo na nabii wa uongo. Pamoja na kuwa msemaji wao, sanamu hiyo pia itahukumu kifo wale wanaokataa kuabudu jozi lisilotakatifu. Katika ulimwengu wetu wa teknolojia, si vigumu kufikiria hali kama hiyo.

Yeyote yule nabii wa uongo anageuka kuwa, udanganyifu wa mwisho wa dunia na uasi wa mwisho utakuwa mkubwa, na ulimwengu wote utachukuliwa ndani yake. Wadanganyifu na walimu wa uongo tunaowaona leo ni watangulizi wa Mpinga Kristo na nabii wa uongo, na hatupaswi kudanganywa na wao. Waalimu hawa wa uongo wamejaa, nao wanatupeleka kuelekea ufalme wa mwisho wa Shetani. Tunapaswa kutangaza injili ya kuokoa ya Yesu Kristo kwa uaminifu na kuokoa roho za wanaume na wanawake kutokana na msiba ujao.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nani nabii wa uongo wa nyakati za mwisho?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries