settings icon
share icon
Swali

Ni jinsi gani Kanisa ni Mwili wa Kristo?

Jibu


Maneno "Mwili wa Kristo" ni mfano wa kawaida wa Agano Jipya kwa Kanisa (wote waliookolewa kweli). Kanisa linaitwa "mwili mmoja katika Kristo" katika Warumi 12: 5, "mwili mmoja" katika 1 Wakorintho 10:17, "mwili wa Kristo" katika 1 Wakorintho 12:27 na Waefeso 4:12, na "mwili" katika Waebrania 13: 3. Kwa wazi Kanisa linalinganishwa na "mwili" wa Kristo katika Waefeso 5:23 na Wakolosai 1:24.

Wakati Kristo alipoingia ulimwenguni, alichukua mwili wa asili "ulioandaliwa" kwake (Waebrania 10: 5; Wafilipi 2: 7). Kupitia mwili wake wa asili, Yesu alionyesha upendo wa Mungu kwa uwazi, kwa hakika, na kwa ujasiri — hasa kwa njia ya kifo cha dhabihu msalabani (Warumi 5: 8). Baada ya kupaa kwake kwa mwili, Kristo anaendeleza kazi Yake duniani kwa njia ya wale aliowakomboa — Kanisa sasa linaonyesha upendo wa Mungu wazi, kwa hakika, na kwa ujasiri. Kwa njia hii, Kanisa hufanya kazi kama "Mwili wa Kristo."

Kanisa linaweza kuitwa Mwili wa Kristo kwa sababu ya ukweli huu:

1) Wanachama wa Mwili wa Kristo wamejiunga na Kristo katika wokovu (Waefeso 4: 15-16).

2) Wanachama wa Mwili wa Kristo wanamfuata Kristo kama Mchungaji wao (Waefeso 1: 22-23).

3) Wanachama wa Mwili wa Kristo ni uwakilishi wa kimwili wa Kristo katika ulimwengu huu. Kanisa ni kiumbe ambacho Kristo anaonyesha maisha yake kwa ulimwengu hii leo.

4) Wajumbe wa Mwili wa Kristo wanajazwa na Roho Mtakatifu wa Kristo (Warumi 8: 9).

5) Wajumbe wa Mwili wa Kristo wana vipaji vya aina mbalimbali vinavyofaa kwa kazi fulani (1 Wakorintho 12: 4-31). "Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo" (mstari wa 12).

6) Wanachama wa Mwili wa Kristo hushirikisha Wakristo wengine wote, bila kujali historia, rangi, au huduma. ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe" (1 Wakorintho 12:25).

7) Wanachama wa Mwili wa Kristo wako salama katika wokovu wao (Yohana 10: 28-30). Ili Mkristo apoteze wokovu wake, Mungu atakuwa ana "ukata" Mwili wa Kristo!

8) Wanachama wa Mwili wa Kristo hushirikia katika kifo na ufufuo wa Kristo (Wakolosai 2:12).

9) Wanachama wa Mwili wa Kristo wanashiriki katika urithi wa Kristo (Warumi 8:17).of the Body

10) Wanachama wa Mwili wa Kristo wanapokea karama ya haki ya Kristo (Warumi 5:17).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni jinsi gani Kanisa ni Mwili wa Kristo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries