settings icon
share icon
Swali

Je! Biblia inafundisha nini kuhusu jengo la kanisa?

Jibu


Kunazo aina nne za kimsingi za uongozi wa kanisa zilizopo hii leo. Na hizo ni maaskofu, makasisi, kanisa lenye kujitawala, na ule usio na uongozi, lakini ikumbukwe kuwa maneno hayo hayazulutishwi na yale majina yanayokinzana nayo katika madhehebu (kwa mfano, makanisa mengine ya Wabaptisti yatumia uongozi makasisi). Ingawa aina hizi hazijawekwa wazi katika Biblia, tunayo miongozo Fulani ambayo tunaweza kutumia.

Muundo wa kanisa – Kichwa cha kanisa
Ikiwa tungetengeneza mchoro wa shirika, Yesu Kristo ataingia katika nafasi ya Mwanzilishi, Rais, Mkurugenzi Mtendaji, CFO, na Mwenyekiti wa kamati/Bodi. Katika lugha ya kibiblia, Kristo ni "kichwa cha vitu vyote kwa ajili ya Kanisa" (Waefeso 1:22; taz. Wakolosai 1:18) Kanisa ni "ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi" (Waefeso 5:23). Uhusiano wa Yesu na kanisa ni wa karibu sana na ni wa upendo, kwa sababu "Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake" (Waefeso 5:25). Anatamani "apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia" (Waefeso 5:27).

Muundo wa kanisa – Vyeo vya kanisa
Mhubiri (kwa maana halisi, "mchungaji") ni mwanadamu kichwa cha kanisa. Katika kanisa la kwanza, inaonekana kuwa kulikuwa na wingi wa wazee/makasisi, ambao pia huitwa "maaskofu" au "waangalizi." Wazee ndio wanaoongoza kanisa na wana jukumu la kufundisha Neno na kuongoza, kuonya, na kuhimiza watu wa Mungu. (Tazama 1 Timotheo 3: 1-7 na Matendo 14:23.) Mtu anayeshikilia majukumu ya mchungaji / mwalimu hakika ni mmoja wa wazee.

Idara nyingine ni ile ya shemasi. Mashemasi na wanaume ni wanaume wanaoshughulikia maswala ya kanisa, kama vile kutunza wagonjwa, wakongwe, au wajane na kutunza majengo au mali nyingine. (Tazama Matendo 6: 1-6 na 1 Timotheo 3: 8-12.)

Muundo wa kanisa – Uhusiano kati ya idara za kanisa
Mashemasi kwa mara ya kwanza walichaguliwa na kanisa la Yerusalemu (ona Matendo 6). Mitume ambao walisimamia kama wazee huko, waliwachagua mashemasi na kuunda majukumu yao. Kwa hivyo, mashemasi wakati wote wamekuwa chini ya uongozi wa wazee.

Wakati mchungaji anayefundisha anashiriki jukumu la usimamizi wa kiroho pamoja na wazee wengine wa kanisa, Paulo anaonyesha kuwa cheo hicho hubeba jukumu la ziada. "Wazee wa kanisa wanaoongoza shughuli za kanisa vizuri wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhubiri na kufundisha" (1 Timotheo 5:17). Kwa hivyo, mchungaji na wazee wengine wanatoshana kimamlaka lakini sio katika majukumu.

Muundo wa kanisa – Uhusiano kati ya makanisa
Paulo ana haja sana jinsi makanisa anuwai yalivyosaidiana, haswa kwa kuwa kila kanisa ni "mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili" (1 Wakorintho 12:27). Paulo aliwasifu Wafilipi kwa kushiriki naye "masuala ya kutoa na kupokea" (Wafilipi 4:15), ambayo inamaanisha kwamba walimsaidia kifedha ili aweze kuimarisha makanisa mengine. Paulo pia aliongoza ukusanyaji wa misaada kwa kanisa lililokuwa na shida huko Yerusalemu (Matendo 24:17; Warumi 15: 26-27; 1 Wakorintho 16: 3; 2 Wakorintho 8-9). Katika Agano Jipya lote, makanisa yalitumiana salamu (1 Wakorintho 16:19), walituma washiriki kutembelea na kusaidia makanisa mengine (Matendo 11:22, 25-26; 14:27), na walishirikiana ili kufikia makubaliano juu ya mafundisho sahihi ya kanisa ( (Matendo 15: 1-35).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Biblia inafundisha nini kuhusu jengo la kanisa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries