settings icon
share icon
Swali

Je, ni makosa kwa mume na mke wakristo kushiriki katika makanisa tofauti?

Jibu


Mume na mke kushiriki katika makanisa tofauti ni hali ambayo ni ya kawaida zaidi kuliko tunavyofikiria. Pia ni kawaida kwa watoto wa wanandoa hao villevile kugawanyika kati ya makanisa mawili, na hivyo kuleta mgawanyiko katika familia ambayo sio mzuri. Ili kuamua ikiwa ni "mbaya" kwa mume na mke kushiriki katika makanisa tofauti, ni lazima tuangalie kwanza ndoa kama uhusiano ulioanzishwa na Mungu.

Mwanzo 2:24 inatuambia kwamba Mungu aliumba mwanamume na mwanamke kuwa "mwili mmoja" wakati wanapofunga ndoa, wala sio viumbe wawili tofauti ambao huenda njia zao tofauti. Kuna umoja katika ndoa ambao ni wa kipekee na takatifu. Aidha, ndoa ni picha ya Kristo na kanisa lake (waumini) kama ilivyoelezwa katika Waefeso 5: 31-32. Agano la ndoa kati ya mwanamume na mwanamke ni mfano wa agano kati ya Kristo na wale aliokufa kwa ajili yao. Agano lake ni la milele na lililo takatifu kama vile ndoa inafaa kuwa takatifu, na isiyovunjika. Umoja huu wa watu wawili kuwa unafikia patakatifu sana katika ulimwengu wa kiroho, ambako wawili wanapaswa kuwa na mawazo moja kuhusu mafundisho ya msingi ya Ukristo — Mungu, Kristo, dhambi, wokovu, mbinguni / kuzimu, nk. Umoja huu wa ufahamu kupitia huduma ya Roho Mtakatifu huunganisha mume na mke katika kifungo cha kipekee duniani.

Ingawa inawezekana kwa mume na mke kuwa na ladha tofauti ya muziki, mitindo ya kuhubiri au ibada, vipindi vya watoto, nk., Hakuna hata moja ya mambo haya yanatosha kuvunja familia katika sehemu mbili ili waweze kuhudhuria makanisa tofauti juu ya maoni tofauti. Ni wazi kwamba kama makanisa mawili yanafuata Biblia na kuheshimu Kristo, hakuna sababu ambayo mwenzi mmoja hawezi kuweka matakwa ya kibinafsi kando. Njia mbadala bora ni kwa wanandoa kujiunga na kanisa ambako Neno la Mungu linahubiriwa kama mwongozo pekee wa imani na matendo, ambapo familia nzima inaweza kujifunza injili ya kweli ya Yesu Kristo, na ambapo familia inaweza kushirikiana na waumini wenye nia moja. Katika jambo hili, mume, kama kiongozi wa kiroho wa familia, anapaswa kuongoza na kufanya uamuzi wa mwisho, kwa upendo akizingatia maoni ya mke wake.

Kwa kusikitisha, familia ya kushiriki katika kanisa mbili mara nyingi hutokea katika ndoa ambapo mwanandoa mmoja alilelewa katika Kirumi Katoliki na mwingine katika dini ya Pentekote. Katika hali kama hizi, ingekuwa ni busara kwa wanandoa kutofunga ndoa. Tafadhali soma makala ifuatayo: Wakristo wa madhehebu tofauti wanapaswa kuoana? Ikiwa ndoa tayari imefanyika, wanandoa wanapaswa kujitahidi kwa umoja wa kiroho. Watu wawili wanaotofautiana katika mafundisho ya dini mara nyingi huwa ni vigumu sana kua na kuafikiana, lakini katika Mungu, vitu vyote vinawezekana. Wanandoa katika hali hiyo wanaweza kulazimika kuhudhuria makanisa tofauti, hasa kama mmoja au wawili hao wanafikiri imani ya mwenzake kuwa isiyo ya kibiblia. Katika hali hiyo, wote wawili wanapaswa kujitolea kuomba kwamba ukweli ufufunuliwe na umoja wa kiroho upatikane.

Migogoro hii ya mafundisho inapaswa kutatuliwa katika familia kabla ya umoja wa kweli kupatikana. Wanandoa wanaoshiriki katika makanisa tofauti wanapaswa kuwa na nia ya kushikilia kila kitu wanachofundishwa hadi kwenye mwanga wa Maandiko na kuwa tayari kuacha kitu chochote kinachopingana na Biblia. Lazima "wajaribu mambo yote; lishikeni lililo jema" (1 Wathesalonike 5:21).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni makosa kwa mume na mke wakristo kushiriki katika makanisa tofauti?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries