settings icon
share icon
Swali

Je! Kuna thamani yoyote kwa mtihani wa vipiwa vya kiriho / hesabu / tathmini?

Jibu


Ni dhahiri kwamba watoto wa Mungu wanastahili kutamani kujua vipawa vya kiroho walizopewa na Roho Mtakatifu kwa kusudi la kumtukuza na kumsifu Mungu (2 Timotheo 1: 6). Wakati huo huo, Biblia haionyeshi ya kwamba vipawa vya kiroho vinaweza kutambuliwa kwa kuchukua mtihani. Tathmini nyingi ya vipawa vya kiroho kimsingi zinafanya kazi sawa. Mtu anayechukua mtihani anajibu tu kwenye orodha ya kauli au maswali. Baada ya maswali yote yamejibiwa, thamani ya namba inatolewa kwa uchaguzi wa majibu, kuhesabiwa, na idadi hiyo huamua ki/vipawa ya kiroho. Kwa kinyume, Biblia inafundisha kwamba Roho Mtakatifu hutoa vipawa vya kiroho kulingana na mapenzi Yake, kulingana na jinsi alivyochagua kutumia mwamini kuwatumikia wengine.

Mojawapo ya shida na mbinu ya mtihani wa vipawa vya kiroho ni kwamba, kati ya Wakristo leo, kuna maoni mengi tofauti juu ya somo lote la vipawa vya kiroho, kama vile ni ngapi ziko, hasa vinavyomaanisha, kama vipawa fulani hazitumiki, na kama tuweza jumuhisha vipawa vya Kristo kwa kanisa lake (Waefeso 4:11) katika orodha ya vipawa vya kiroho. Kwa nadra masuala haya yanazingatiwa katika tathmini hizi. Kuzingatia kwingine ni kwamba, mara nyingi zaidi kuliko, watu huwa wanajiona tofauti na vile wengine huwaona, ambayo inaweza kumaanisha matokeo ya uongo katika tathmini ya vipawa vya kiroho vya mtu.

Tatizo la tatu kwa kutumia njia hii kutambua vipawa vya kiroho ni kwamba vipawa hivi vinatoka kwa Mungu kupitia Roho Mtakatifu, na Roho hutoa vipawa hivo kwa wale anaowachagua (1 Wakorintho 12: 7-11). Katika Yohana 16:13, waumini wanaahidiwa na Yesu kwamba Roho Mtakatifu atawaongoza katika ukweli wote. Inasisitiza kuwa, kwa kuwa ni Roho Mtakatifu ambaye anaamua nani anayepata kipawa gani, Yeye ana hamu zaidi kwetu kujua nini vipawa vyetu kutuliko sisi. Kweli, nia yetu wenyewe ya jinsi sisi "tuna vipawa" mara nyingi ni motisha ya mawazo bure ya umuhimu wetu wenyewe. Kinyume chake, tamaa ya Roho Mtakatifu kwamba tunajua vipawa vyetu vya kiroho daima ni bora, ili tufanye kazi katika mwili kwa namna ambayo huleta utukufu na heshima kwa Baba.

Ikiwa tunatafuta kwa kweli kuongozwa na Mungu kupitia sala, ushirika, kujifunza Neno la Mungu, na mafundisho ya watumishi wa Mungu, vipawa vyetu vitakuwa kawaida. Mungu anatupa tamaa za mioyo yetu (Zaburi 37: 4). Hii haimaanishi kwamba Mungu anatupa chochote tunachotamani — badala yake, anaweza na atatupa tamaa zenyewe. Anaweza kuweka ndani ya mioyo yetu tamaa ya kufundisha, hamu ya kutoa, hamu ya kuomba, hamu ya kutumikia, nk. Wakati tutakapofanya tamaa hizo, na kujitolea kwa kweli kwa utukufu wake katika matumizi ya vipawa vyetu, Matokeo mazuri yatatokea-mwili wa Kristo utajengwa na Mungu atatukuzwa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Kuna thamani yoyote kwa mtihani wa vipiwa vya kiriho / hesabu / tathmini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries