settings icon
share icon
Swali

Kwa nini Wakristo wengi hawana mtazamo wa kibiblia mara kwa mara?

Jibu


Mtazamo wa kibiblia kwa jumla ni jinsi mtu anavyoutizama ulimwengu kutoka kwa mtazamo wa kibiblia. Ni mfumo wa imani ya Kikristo kuhusu maana ya maisha, asili ya Mungu, chanzo cha ukweli, na dhana nyingine za msingi. Hata hivyo, maoni ya Wakristo wengi sio thabiti kibiblia. Wanaweza kukabiliana na masuala fulani kutoka kwa mtazamo wa kibiblia, lakini sio kila suala.

Kuna uwezekano wa sababu nyingi ni kwa nini Wakristo wengine hawawezi kuwa na mtazamo thibit wa kibiblia:

1) Hawajui kile Biblia inasema. Hawajui Neno. Ikiwa mtu hajui Biblia inasema nini juu ya utakatifu wa maisha ya mwanadamu, kwa mfano, itakuwa vigumu kwake kuunda mtazamo wa kibiblia juu ya jambo hilo. Kwa wale ambao hawajui kuwa elimu ni muhimu.

2) Wanakataa kile Biblia inasema juu ya masuala fulani. Ikiwa Mkristo anayesema haamini kile ambacho Biblia inasema, haiwezekani kwake kuwa na mtazamo wa kweli wa kibiblia. Kwa wale ambao ni wako kinyume na kile biblia inasema, toba ni muhimu kwao.

3) Wao wana wasiwasi zaidi na kile ambacho ulimwengu unafikiria kuliko kile ambacho Mungu anafikiria. "Kuwaogopa wanadamu huleta mtego" (Mithali 29:25). Muumini ambaye anauona ulimwengu kutokana na mtazamo wa kibiblia anajua kwamba yeye si wa ulimwengu. Yesu akasema, "Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia" (Yohana 15:19; tazama pia Yohana 17:14). Wakati muumini anaanza kufanya maelewano na njia ya ulimwengu ya kufikiri, anapoteza mtazamo wa Mungu. Kwa wale ambao wanaogopa, ujasiri ndio ufunguo.

4) Wao ni vuguvugu katika kujitoa kwao kwa Kristo. Kama kanisa la Laodikia, "hu baridi wala hu moto" (Ufunuo 3:15), hawataki kuchukua msimamo katika Kristo. Kwa kuvua, kujitolea ni ufunguo.

5) Wao huathiriwa na uongo wa ulimwengu. Kutoka wakati wa Adamu na Hawa, Shetani ametumia uwezo wake wa kudanganya na kuchanganya (Mwanzo 3: 1-7; Ufunuo 12: 9). Chombo chenye nguvu katika silaha za Shetani ni wazo kwamba Biblia ni kitabu cha hadithi, ambacho kwamba kimejaa makosa na hakifai kuaminika. Shetani anataka kuwashawishi watu kwamba Biblia haifai tena, kwamba sheria zake na kanuni zake hazijalishi. Wengi katika kanisa wameathiriwa na mawazo hayo. Kwa wale wamedanganywa, ufahamu ndio jibu.

6) Wao wameyumbishwa na hali yao na kutilia shaka ahadi za Mungu. Katika Mathayo 14 wakati, Petro alipotoka katika mashua na kutembea juu ya maji, alikuwa anaonyesha mtazamo wa kibiblia: Yesu ndiye chanzo cha nguvu zote. Hata hivyo, Petro alipoangazia bahari iliyopigwa na dhoruba, mtazamo wake wa kibiblia ulibadilika: labda mawimbi ni ya nguvu zaidi kuliko Yesu. Kwa wenye shaka, imani ni ufunguo.

Ili uwe na mtazamo wa Kibiblia mara kwa mara tunapaswa kurudi kwenye Biblia na kuzingatia ahadi ambazo Mungu ametupatia, kwa maana dunia haitupi chochote (Luka 9:25, Yohana 12:25, Mathayo 6:19).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kwa nini Wakristo wengi hawana mtazamo wa kibiblia mara kwa mara?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries