settings icon
share icon
Swali

Nimefanya dhambi ya _____ Je! Mungu atasamehe?

Jibu


Jaza dhambi zozote ulizofanya katika pengo ______. Ndiyo, Mungu anaweza kusamehesameha yoyote ile. Mafundisho ya upatanisho yaanaelezea wokovu na msamaha wa dhambi. Mungu alitoa haki ya Kristo kwa wale ambao kwa unyenyekevu wanaomba msamaha wa dhambi (Isaya 53: 5-6; 2 Wakorintho 5:21). Alilipa bei kamili ya dhambi zetu, na waumini wamamesamehewa kikamilifu kwa kila dhambi wanazofanya-zilizopita, za sasa, na za baadaye. Pia kuna msamaha kila siku tunapokiri dhambi zetu na kuacha kwa ajili ya utakaso wetu. Ikiwa unalinganisha dhambi yoyote na mauaji ya Yesu, haiwezi kulinganisha, lakini Yesu alisema, "Baba, wawasamehe kwa maana hawajui wanayofanya" (Luka 23:34).

Dhana ya wokovu na msamaha ina uhusiano mwingi. Kwa bahati nzuri, neema ya Mungu inatosha kwa dhambi yoyote na yote, dhambi yoyote unayoweka katika pengo. Kupokea msamaha ni kwa mtu binafsi. Hiyo ni suala la kwanza; Je, utapokea wokovu (msamaha wa dhambi) ambayo Kristo anatoa? Ikiwa jibu ni "Ndiyo," basi unasamehewa deni zote za dhambi kabisa (Matendo 13: 38-39). Msamaha huu unakuja kwa imani katika Yesu na neema ya Mungu peke yake, si kwa kazi au matendo mema (Warumi 3: 20,22). Wokovu huanza kwa unyenyekevu kukubali kwamba hatuwezi kuwa wazuri kungia mbinguni kwa sifa yetu wenyewe na kwamba tunahitaji msamaha. Kukubali Yesu Kristo inamaanisha kuamini kwamba kifo chake na ufufuo wake ulilipa adhabu ya dhambi zote zilizofanyika na kwamba ni ya kutosha kufunika dhambi zote (2 Wakorintho 12: 9).

Kwa hiyo, ikiwa umempokea Yesu Kristo kama Mwokozi wako, Mungu amesamehe dhambi zako zote. Ikiwa hujafanya hivyo, kiri dhambi zako kwa Mungu, naye atakusafisha na kukurudisha kwa ushirika na kushiriki naye (1 Yohana 1: 8-9). Hata kwa msamaha, bado huenda ukahisi hatia. Kujisikia hatia juu ya dhambi ni jambo la kawaida kwa sababu ya dhamiri yetu, na kazi yake ni kutukumbusha tusije tukarudia mifumo ya dhambi. Kuelewa kwamba Yesu anaweza kusamehe kipimo chochote cha dhambi ni tumaini la wokovu wetu. Kuelewa msamaha ni tiba ya hisia za hatia.

Kujua kwamba msamaha ni kweli kitu kizuri, zawadi nzuri kutoka kwa Mungu anayetupenda inatuwezesha kuona jinsi Yeye ni wa ajabu sana. Tunapotafakari dhambi zetu wenyewe na jinsi hatustahili msamaha, inakuwa dhahiri kwamba Mungu ni mwenye upendo, mwenye huruma, na anastahili ibada yetu. Kiburi cha dhambi ambacho kinakataa kuomba msamaha ni kile kinachosimama kati yetu na uhusiano na Mwokozi mwenye kujali. Lakini kwa wale wanaoomba msamaha, wanaweza kuamini kwamba Yesu anatosha na ana hamu ya kusamehe na kuwaokoa kutoka kwa dhambi zao, na hatimaye wataingia milangoni pake kwa sifa (Zaburi 100: 4).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nimefanya dhambi ya _____ Je! Mungu atasamehe?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries