settings icon
share icon
Swali

Nini kilichotokea katika Mnara wa Babeli?

Jibu


Mnara wa Babeli umeelezwa katika Mwanzo 11: 1-9. Baada ya gharika, Mungu aliamuru binadamu "kuongezeka kwa idadi na kujaza dunia" (Mwanzo 9: 1). Binadamu uliamua kufanya kinyume kabisa: "Wakasema, haya, na tujijengee mji. Na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote"(Mwanzo 11: 4). Binadamu aliamua kujenga jiji kubwa na wote kukusanyika huko. Waliamua kujenga mnara mkubwa kama ishara ya nguvu zao, kujifanyia jina wao wenyewe (Mwanzo 11: 4). Mnara huu unakumbukwa kama Mnara wa Babeli.

Kwa kujibu, Mungu alichanganya lugha za binadamu ili wasiweze kuwasiliana tena na kila mmoja (Mwanzo 11: 7). Matokeo yake ni kuwa watu walikusanyika pamoja na watu wengine ambao walizungumza lugha sawa, kisha wakaenda pamoja na kukaa katika sehemu nyingine ya dunia (Mwanzo 11: 8-9). Mungu alichanganya lugha kwenye Mnara wa Babeli ili kutekeleza amri yake kwa binadamu kuenea ulimwenguni pote.

Baadhi ya walimu wa Biblia pia wanaamini kwamba Mungu aliumba jamii tofauti za binadamu kwenye Mnara wa Babeli. Hii inawezekana, lakini haifundishwi katika maandiko ya kibiblia. Inaonekana zaidi kwamba jamii tofauti zilikuwepo kabla ya Mnara wa Babeli na kwamba Mungu alichanganya lugha, angalau sehemu, kulingana na jamii tofauti. Kutoka Mnara wa Babeli, binadamu aligawanyika kulingana na lugha (na uwezekano wa jamii) na kukaa katika maeneo mbalimbali duniani.

Mwanzo 10: 5, 20 na 31 hufafanua uzao wa Nuhu kuenea juu ya dunia "kwa jamaa zao na lugha, katika maeneo yao na mataifa." Je! Hii inawezekanaje, kwa kuwa Mungu hakuchanganya lugha hadi Mnara wa Babeli katika Mwanzo sura ya 11? Mwanzo 10 inataja uzao wa wana watatu wa Nuhu: Shemu, Hamu, na Yafethi. Inataja wazao wao kwa vizazi kadhaa. Kwa muda mrefu wa maisha ya wakati huo (angalia Mwanzo 11: 10-25), ukoo wa kizazi katika Mwanzo 10 inawezekana kufunika mamia kadhaa ya miaka. Maelezo ya Mnara wa Babeli, iliyoelezwa katika Mwanzo 11: 1-9, inatoa maelezo zaidi juu ya wakati ambapo lugha zilichanganyikiwa. Mwanzo 10 inatuambia lugha tofauti. Mwanzo 11 inatuambia jinsi lugha tofauti zilivyoanza.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nini kilichotokea katika Mnara wa Babeli?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries