settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kumwamini Mungu wakati ninakabiliwa na ukosefu wa ajira, kuchukuliwa kwa mali baada ya kushindwa kulipa mkopo, au kufilisika?

Jibu


Hasara ya ajira na/au kipato ni moja ya matukio ya kuhuzunisha zaidi katika maisha, hasa kwa wale wanaokimu familia. Kuchukuliwa kwa mali baada ya kushindwa kulipa mkopo juu ya nyumba ya familia au kutangaza kufilisika kwa sababu ya ukosefu wa ajira huongeza hofu ya ziada, kutokuwa na uhakika, na machafuko ya kihisia. Kwa mwanaume au mwanamke Mkristo anayekabiliwa na ukosefu wa ajira, kuchukuliwa kwa mali baada ya kushindwa kulipa mkopo au kufilisika, kunaweza kuwa na mashaka zaidi kuhusu wema wa Mungu na ahadi Zake za kutoa kwa watoto Wake. Je! Mkristo anawezaje kujibu kwa matukio haya ya maisha ya balaa? Ni kanuni gani za kibiblia ambazo tunaweza kutumia kwa kupoteza nyumba au kazi na faida (bima ya afya/maisha, kustaafu)?

Kwanza, ni muhimu kuelewa kwamba Mungu ameamuru kazi kwa wanadamu. Kazi inaelezwa katika Biblia kama yenye manufaa kwa kuwa inatoa kwa mahitaji yetu (Methali 14:23; Mhubiri 2:24, 3:13, 5:18-19) na inatupa rasilimali za kushirikiana na wengine wanaohitaji (Waefeso 4:28). Paulo aliwakumbusha waumini huko Thesalonike kwamba mtu yeyote ambaye hakutaka kufanya kazi asipate kula (2 Wathesalonike 3:10) na kwamba yeye mwenyewe alifanya kazi kwa kutengeneza hema ili asiwe mzigo kwa mtu yeyote (Matendo 18:3; 2 Wakorintho 11:9). Hivyo, kupoteza ajira haipaswi kuwa sababu ya uvivu, na kwa bidii zote zinazofaa zinapaswa kutumika ili kupata ajira nyingine haraka iwezekanavyo (Methali 6:9-11).

Wakati huo huo, inaweza kuwa haiwezekani kupata nafasi sawa katika malipo na hali kwa ile iliyopotea. Katika matukio haya, Wakristo hawapaswi kuruhusu kiburi kuwazuia kuchukua kazi katika maeneo mengine, hata ikiwa ina maana ya hali ya chini au malipo kidogo, angalau kwa muda. Tunapaswa pia kuwa tayari kukubali msaada kutoka kwa waumini wengine na makanisa yetu, labda badala ya kazi ambazo zinahitajika kufanywa katika manyumba, ua, na nyenzo za kanisa. Kupanua na kukubali "mkono wa kusaidia" katika nyakati hizi ni baraka kwa wale wanaotoa na wale wanaopokea na kuonyesha "sheria ya Kristo," ambayo ni kupendana (Wagalatia 6:2; Yohana 13:34).

Vilevile, hata kupoteza nyumba ya familia kwa njia ya kuchukuliwa baada ya kushindwa kulipa mkopo au kufilisika inaweza kuwa wakati wa baraka kwa familia, wakati ambapo wazazi na watoto "kufunga vyeo" na kuwa na ufahamu mkubwa zaidi wa upendo wao kwa kila mmoja na mambo muhimu katika maisha — imani, jamii na jumuia — na kuzingatia kwa chini vitu vya kimwili ambavyo havina thamani ya milele na vinaweza kutoweka kwa muda mfupi. Mungu anaweza pia kutumia hali hizi kutukumbusha ukweli uliozunguzwa na Yesu katika Mathayo 6:19-20 na kufanya tena mioyo yetu juu ya hazina ya mbinguni.

Zaidi ya yote, kufanya upya imani na matumaini yetu katika ahadi za Mungu ni muhimu sana wakati wa matatizo ya kifedha. Kurejelea tena vifungu ambavyo vinavyosema uaminifu wa Mungu kwa watoto Wake vitatupa nguvu na kutuhimiza wakati ujao unavyoonekana kuwa mkali. 1 Wakorintho 10:13 inatukumbusha kwamba Mungu ni mwaminifu na hatatujaribu zaidi ya uwezo wetu wa kuibeba na atatoa njia ya kutoka kwa majaribu. Hii "njia ya kutoka" inaweza kumaanisha kazi mpya na bora inayofunguka mara moja. Inaweza pia kumaanisha muda mrefu wa ukosefu wa ajira wakati ambapo uaminifu wa Mungu katika kutoa mkate wetu wa kila siku unaonyeshwa kwetu. Inaweza kumaanisha nyumba mpya, au inaweza kumaanisha kuishi katika hali iliyopunguzwa na jamaa kwa kipindi cha muda fulani. Katika kila kesi, njia ya kutoka kwa kweli ni "njia kupitia" jaribio, ambayo tunajifunza juu ya utoaji waaminifu wa Mungu vile Anatembea kwa upande wetu kupitia mateso yote. Wakati wa kipindi cha kujaribu kimekwisha, imani yetu itaimarishwa, na tutaweza kuimarisha wengine kwa kutoa ushuhuda wenye nguvu juu ya uaminifu wa Mungu wetu.

English


Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kumwamini Mungu wakati ninakabiliwa na ukosefu wa ajira, kuchukuliwa kwa mali baada ya kushindwa kulipa mkopo, au kufilisika?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries