settings icon
share icon
Swali

Mizimu waliokuwa jela ni kina nani?

Jibu


"Mizimu gerezani" wanatajwa katika muktadha wa kile Yesu alichofanya wakati wa kufa kwake na ufufuo. Petro wa kwanza 3: 18-20 inasema, " Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa, ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;

Watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa.'' Kumbuka kwamba mwili wa Yesu ulikufa na ulisubiri ufufuo, lakini alikuwa hai katika kiroho wakati alipotembelea mizimu jela. Kwa kurejelea muktadha, tafadhali soma makala yetu juu ya "Yesu alikuwa wapi siku tatu kati ya kifo chake na ufufuo?"

Tunajua mambo manne kuhusu mizimu wanaotajwa katika 1 Petro 3:19. Ni wasio wa kawaida, wamefungwa, dhambi yao ilifanyika kabla ya Mafuriko, na Yesu alitembelea mahali pao pa uhamisho ili awape ujumbe. Haijulikani mizimu hawa walikuwa nani na jambo hili limezua fikra tofauti kwa miaka mingi.

Kwanza, hebu tuangalie neno 'roho'. Ni tafsiri ya neno la Kiyunani pneumasin, aina ya neno pneuma, ambayo ina maana "hewa, pumzi, upepo." Inatumika katika Agano Jipya kutaja malaika (Waebrania 1:14), mapepo (Marko 1: 23), roho wa Yesu (Mathayo 27:50), Roho Mtakatifu (Yohana 14:17), na sehemu ya kiroho ya mwanadamu (1 Wakorintho 2:11). Biblia inaeleza kwamba wanadamu wana roho (Waebrania 4:12), Bibilia inarejelei watu kuwa "pepo" tu. Kwa kinyume chake, Mungu Roho Mtakatifu, malaika, na pepo hawana kamwe kuwa na roho; wao ni roho. Hivyo maana ya kawaida ya mizim katika muktadha mizimu iliyo gerezani inamaanisha mizimu ni kitu kingine wala sio wanadamu.

Mizimu gerezani haiwezi kuwa Malaika watakatifu, kwa sababu hawajafanya dhambi na hawajafungwa. Na, kama mizimu walio gerezani si roho za wanadamu waliokufa, ina maana ya kwamba mizimu za gereza ni mapepo. Sasa, ni dhahiri kwamba sio pepo wote waliofungwa. Agano Jipya inatoa mifano mingi ya shughuli za pepo duniani. Hivyo,mizimu walio gerezani ni lazima ziwe kikundi cha pepo ambacho wamefungwa, tofauti na pepo wengine wa ushirika wao.

Je! Ni kwa nini pepo wengine wamefungwa bali sio wote? Yuda 1: 6 inatupa ufunuo muhimu: "Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu." Kuna baadhi ya malaika walioanguka waliofanya uhalifu mbaya wa aina fulani; Yuda 1: 6 haitoi maelezo, bali dhambi za pepo zilihusiana na jinsi ambavyo "hazikuweka nafasi yao wenyewe bali zimeacha makao yao mazuri." Ufunuo 9: 1-12, 14-15, na 2 Petro 2: 4 pia huzungumzia juu ya kundi la malaika waovu sana ambao sasa wamefungwa.

Dhambi zilizotendwa na mizimu walio gerezani inaweza kuwa sawa na dhambi inayotajwa katika Mwanzo 6: 1-4, ambayo inasema "wana wa Mungu" kujihusisha kimapenzi na "binti za wanaume" na kuzalisha kizazi kikubwa, Wanefili. Ikiwa "wana wa Mungu" walikuwa malaika walioanguka, basi dhambi ya Mwanzo 6 inahusisha malaika kuondoka mahali ambapo walikuwa katika tendo la kutotii kabla ya gharika — na hiyo inafanana na kile mtume anachosema katika 1 Petro 3:19. Inaonekana inawezekana kwamba pepo waliokuwa wakishirikiana katika ngono na wanawake wa kibinadamu walifungwa na Mungu kuwazuia kurudia dhambi hiyo na kuwakataza wale mapepo wengine wasijaribu.

Kulingana na 1 Petro 3:19, Yesu "alitangazia" mizimu katika jela. Neno lililotafsiriwa "kutangazwa" au "kuhubiriwa" linamaanisha "kutangaza kwa umma" au "kuhubiri." Petro anasema kwamba Yesu alikwenda gerezani na kutangaza ushindi wake kwa malaika walioanguka na waliofungwa huko. Walishindwa, na Yeye alikuwa ameshinda. Msalaba unashinda uovu wote (tazama Wakolosai 2:15).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mizimu waliokuwa jela ni kina nani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries