settings icon
share icon
Swali

Je! Watu huko mbinguni wanaweza kutuangalia chini na kutuona wale tungali bado duniani?

Jibu


Waebrania 12:1 yasema, “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii….” wengine wanaelewa “wingu kuu la mashahidi” kuwa watu ambao wanaangalia chini kutoka mbinguni. Hii sio fasiri nzuri. Waebrania mlango wa 11 yarekodi watu wengi ambao Mungu aliwapongeza kwa imani yao. Ni watu hawa ambao wako katika “wingu la mashahidi.” Wao ni “mashahidi” sio kwamba wanatuchungulia, bali kwa hayo wamekwisha tuwekea mfano. Wao ni mashahidi wa kristo na Mungu na kweli. Waebrania 12:1 yaendelea “….na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yatu.” Kwa sababu ya imani na hekima ya Wakristo ambao walitutangulia, lazima tutiwe moyo kwa kufuata mfano wao.

Bibilia haitaji hasa kama watu mbinguni wanatuangalia au hawatuangalii wale sisi tuko katika ulimwengu. Ni vile pengine wanaweza kufanya hivyo. Ni kwa nini? Kwanza wakati mwingine wanaona vitu ambavyo vitawafanya wasikitike na kuhisi uchungu kwa mfano, matendo ya dhambi na uovu. Kwa vile hakuna husuni, machozi, ama kasiriko mbinguni (Ufunuo 21:4), haionekani kuwa inawezekana kuona yanayochiri ulimwenguni. Pili, watu mbinguni wote wako katika ibada wakimwabudu mungu na kufurahia utukufu wa mbinguni kiwango inaonekana kuwa watakuwa na haja na chenye kinaendelea duniani. Kwa madhumuni kwamba wako huru kutoka dhambi na kuhisi uwepo wa bwana mbinguni hiyo peke yatosha kuchangamsha mawazo yao. Pia ikiwa uwezekano kuwa Mungu huko mbinguni anawaruhusu kuwalinda waenzi wao, Bibilia haitupi sababu yoyote ya kuonyesha kuwa kweli haya yalitokea.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Watu huko mbinguni wanaweza kutuangalia chini na kutuona wale tungali bado duniani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries