settings icon
share icon
Swali

Mbegu ya imani ni nini? Ni nini kutoa sadaka ya imani?

Jibu


Watetezi wa "uinjilisti wa ustawi" na vuguvugu la Neno la Imani mara nyingi hupenda kuzungumza juu ya "mbegu," "sadaka ya imani ya mbegu," na "kupokea mara dufu." Sadaka ya mbegu ya imani ni fedha iliyotolewa kwa imani kwamba Mungu ataizidisha na kuirudisha kwa mtoaji. Vile unavyo toa fedha Zaidi -na kuwa na imani zaidi -ndivyo utapata pesa nyingi. Wahubiri wa ustawi mara nyingi huomba saka kwa huduma zao kwa kuahidi kwamba kwa aina hiyo tutazidishiwa: "Nitumie $ 10 na uamini Mungu kuwa atakupa $ 1,000." Wanaitisha fedha kwa udanganyivu wa kiroho kwa maneno kama "Mungu anataka kukubariki na muujiza "na" Yesu ni mkubwa kuliko deni lako." Na watatumia vibaya mistari kama vile Marko 4: 8,"Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia." Ni vizuri kumbuka "mbegu" katika aya hii ni Neno la Mungu (Marko 4:14), sio fedha.

Marehemu Oral Roberts alikuwa na ushawishi mkubwa sana katika kueneza dhana ya sadaka ya mbegu ya imani, na aliwafundisha watu kutarajia muujiza wakati wanapanda "mbegu" kutokana na "mahitaji yao." Aliandika, "Ili utambue uwezo wako, ushinde matatizo ya maisha, kuona maisha yako yakiwa na matunda, kuongezeka na kutoa kwa wingi (yaani afya, ustawi, upya wa kiroho, katika familia au mwenyewe), unapaswa kuamua kufuata sheria ya Mungu ya mkulima na mavuno. Panda mbegu ya ahadi yake sehemu ya mahitaji yako" (kutoka "Kanuni za Mbegu "). Katika toleo la Julai 1980 la Maisha mengi, Roberts aliandika, "Tatua mahitaji yako ya fedha na mbegu za fedha" (ukurasa wa 4).

Richard Roberts, mwana wa Oral, anasema kwenye tovuti yake, "Mpe Mungu kitu cha kufanya kazi nacho. Haijalishi ni kidogo kiasi gani vile unavyo fikiri, panda kwa furaha na imani, ukijua moyoni mwako unapanda mbegu ili uweze kuvuna miujiza. Kisha uanze kutarajia aina zote za miujiza! "Mnamo Mei 2016, jarida la Roberts liliomba rufaa za fedha kwa maneno haya:" Panda mbegu maalum $ 100. . . . Ikiwa utapanda mbegu hii nje ya mahitaji yako na kuingia mkataba mkamilifu na mimi, basi pamoja na wewe tutatarajia MUUJIZA MKUU KUTOKA KWA MWENYEZI MUNGU" (kutoka kwenye tovuti yake, msisitizo wa awali).

Kulingana na Oral Roberts, njia ya kuchukua faida ya sheria ya kupanda na kuvuna ni mara tatu: 1) Mtazamie Mungu kama chanzo chako, 2) Toa kwanza ili uweze kupokea, na 3) Tarajia muujiza. Kama "maandishi ya ushahidi" kwa hatua ya pili, walimu wa mbegu ya imani wanatumia Luka 6:38, "Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa." Matumizi mabaya ya aya hii huanza na matumizi yake kwa faida ya kimwili — Yesu alikuwa akizungumzia hasa msamaha katika Luka 6:37, sio fedha. Pia, kuna tofauti kati ya "Toa, na" na "Toa ndio." Waalimu wa mbegu ya imani wanasisitiza lengo la ubinafsi la kutoa-kutoa ili uweze kupata-na wanasema mengi. Biblia inafundisha kwamba tunatoa kwa ajili ya kuwafaidi wengine na kumtukuza Bwana, sio kujitajirisha wenyewe.

Walimu wa dhabihu ya mbegu ya imani kama vile Mathayo 17:20, "Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu." Bila shaka, aya hii haisemi chochote kuhusu kupata pesa au kutoa sadaka ya mbegu ya imani.

Kifungu kingine kilichotumiwa vibaya na wahubiri wa mbegu ni Marko 10: 29-30, "Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili, ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele." Waalimu wa mbegu wanatazama ahadi ya "mara mia moja," lakini huitumia tu kwa "nyumba" na "mashamba" -iyo ni utajiri wa mali. Wanapuuza orodha inayofuata yote. Je, tuseme kwamba Yesu aliwaahidi wafuasi wake mama halisi wa kweli au kwamba tunapaswa kutarajia marafiki zaidi wa damu kuliko tulio nao sasa? Au Yesu alikuwa anazungumzia familia ya kiroho iliyoongezeka? Kwa kuwa mama na baba na ndugu na dada ni wa kiroho, labda nyumba na mashamba ni kiroho, pia.

Wafuasi wa mafundisho ya sadaka ya imani ya mbegu hupuuza maelezo kadhaa muhimu katika Maandiko. Fikiria, kwa mfano, 2 Wakorintho 9: 10-12, "Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;

11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu." Kifungu hiki kinasema Mungu anatoa mbegu za kupanda; yaani, Anatupa rasilimali kwa ajili yetu ili tutoe kwa ukarimu. Na, tunapompa, Mungu atatoa rasilimali zaidi ili tuendelee kutoa. Kumbuka, hata hivyo, uvunaji sio faida ya fedha bali "mavuno ya haki yako." Pia, ni shukrani kwa Mungu ambayo inabubujika, sio akaunti zetu za benki. Mbegu iliyopandwa katika kifungu hiki haisababishi miujiza au utajiri wa kibinafsi.

Wafuasi wa sadaka mbegu ya imani pia hupuuza ukweli kwamba mitume hawakuwa watu matajiri. Mitume hakika aliwapa wengine: "Nami kwa furaha nyingi nitatapanya, tena nitatapanywa kwa ajili ya roho zenu..." (2 Wakorintho 12:15). Kulingana na mafundisho ya sadaka ya mbegu ya imani, Paulo lazima alikuwa tajiri. Hata hivyo, "Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tu uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao" (1 Wakorintho 4:11). Mitume walikuwa masikini, huku wakiwa wabarikiwa wa kiroho na Bwana.

Mungu anapenda anayetoa kwa furaha (2 Wakorintho 9: 7), lakini hatupaswi kudhani kuwa neema yake itaonyeshwa katika kuzidishiwa fedha. Wala hatupaswi kusingizia ahadi zilizopewa Agano la Kale kwa Israeli kuwa zetu wenyewe. Lengo letu la kutoa haliipaswi kukuwa kupata pesa mara dufu. Lengo letu linapaswa kuwa utakatifu na ustahili (ona 1 Timotheo 6: 6-10). Tunapaswa kuomba, "Bwana, nisaidie kujifunza kuwa na maudhui na yale niliyo nayo, hata kama nina njaa au nina mahitaji" (ona Wafilipi 4: 11-13).

Mafundisho ya mbegu ya imani kwa kiasi kidogo zaidi huwa ni mpango wa kupata-utajiri wa haraka ambao hufionza wale ambao wamekata tamaa na wanaoumia kati ya watu wa Mungu. Petro alilionya kanisa juu ya hila kama hiyo: "Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa..." (2 Petro 2: 3).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mbegu ya imani ni nini? Ni nini kutoa sadaka ya imani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries