settings icon
share icon
Swali

Je, kuzikwa ndio chaguo pekee Mkristo anaweza kuzingatia?

Jibu


Wakristo wengi kwa karne nyingi walitaka kuzikwa baada ya kifo na sherehe inayotangaza ujumbe wa ufufuo; kwamba sherehe, iliyo na ibada na mila mbalimbali, imejulikana kama "mazishi ya Kikristo." Kuna njia nyingine zaidi ya kuzikwa kwa Wakristo kuzingatia; kuchujwa/kuchomwa, ingawa haichukuliwi kuwa njia ya "jadi" ya mazishi, walakini imkuwa na maarufu zaidi.

Kuzikwa kwa Kikristo sio neno la wazi katika kibiblia. Biblia haitoi maagizo juu ya jinsi mwili unapaswa kushughulikiwa baada ya kifo. Katika tamaduni za nyakati za Biblia, kuzikwa katika kaburi, pango, au chini ilikuwa njia ya kawaida ya kuondoa mwili wa mwanadamu (Mwanzo 23:19; 35: 19-20, 29; 2 Mambo ya Nyakati 16:14; Mathayo 27: 60-66). Njia ya kawaida ya mazishi katika Biblia ilikuwa kuwaweka wafu ndani ya makaburi ya juu, kwa wale ambao wangeweza kulipa. Kwa wale ambao hawakuweza kumudu, miili ilikuwa imefungwa chini. Katika Agano Jipya, makaburi ya juu ya ardhi yalikuwa bado yamehifadhiwa kwa maziko ya matajiri. Ndio maana Yesu, ambaye hakuwa na utajiri wa kidunia, alizikwa katika kaburi lililokopwa (Mathayo 27: 57-60).

Kuzingatia sheria za nchi hii kuhusu maiti ni jambo muhimu. Sheria hutofautiana kutoka nchi hadi nchi na ndani ya mikoa ya nchi hizo. Kwa sababu Wakristo wanapaswi kutii mamlaka ya serikali, sheria zinazohusiana na jinsi ya kuuweka mwili. Kisha kuna swali la maziko ya Kikristo dhidi ya kuchoma. Wala sio amri katika Biblia, wala kukataliwa. Ukweli kwamba Wayahudi na Wakristo wa mapema walifanya maziko pekee inakutosha kuwashawishi watu wengine kuchagua maziko hii leo. Na ukweli kwamba mara tu Biblia inasema kuwa wafu kuchomwa moto ni katika mazingira ya waovu kuadhibiwa kwa makosa yao (Mambo ya Walawi 20:14; Yoshua 7:25) pia inawashashi wengine kukataa kuchoma wafu. Lakini, tena, Wakristo hii leo hawana amri ya Biblia ya wazi au dhidi ya kuchoma. Mwishoni, ni bora kuachia uamuzi huo kwa familia ya marehemu.

Njia inayotumiwa kuuondoa mwili sio muhimu sana kama ukweli wa dhana ya maziko ya Kikristo: kwamba mwili haubebi tena mtu aliyekufa. Paulo anaelezea miili yetu kama "hema," yaani, makao ya muda. "Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni" (2 Wakorintho 5: 1). Wakati Yesu atakaporudi, Wakristo watafufuliwa uzima, na miili yetu itabadilishwa kuwa utukufu, miili milele. "Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika; hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguv" (1 Wakorintho 15: 42-43).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, kuzikwa ndio chaguo pekee Mkristo anaweza kuzingatia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries