settings icon
share icon
Swali

Je, Biblia inasema nini kuhusu maungamo ya mwisho?

Jibu


Maelezo ya juu Zaidi ya maungamo ya mwisho / maungamo ya dakika ya mwisho kwa Kristo katika Biblia ni kesi ya mhalifu aliyesulubiwa pamoja na Yesu (Luka 23: 39-43). Mara tu kabla ya kifo chake mwenyewe, mhalifu huyo alikuwa si mwaminifu mkejeli wa Kristo (Mathayo 27:44). Hata hivyo, wakati wa mwisho, huyo mhalifu alitubu na kumkubali Yesu kama Mfalme wa mbinguni. Bwana alimpa ahadi iliyobarikiwa, "Leo utakuwa nami katika Paradiso."

Ingawa hadithi ya mhalifu msalabani inaonyesha kwamba maungamo ya dakika ya mwisho yanawezekana, Biblia inatuonya kutubu sasa, bila kusubiri wakati mwingine. Yohana Mbatizaji alionya, "Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekaribia" (Mathayo 3: 2). Yesu alikuwa na ujumbe wa kufanana kuhusu haja ya toba ya haraka (Mathayo 4:17).

Biblia inatuonya juu ya ufupi wa maisha. "Wewe ni mvuke tu inayoonekana kwa muda kidogo na kisha utoweka" (Yakobo 4:14). Hatuna maagizo ya kufikiria kubadilisha siku fulani, lakini kuamini leo! "Leo mkisikia sauti yake, msiifanye migumu mioyo yenu" (Waebrania 4: 7). Hakuna hata mmoja wetu anayejua ni muda gani tuliosalia katika maisha haya au ni hali gani ya kifo chetu kitakuwa. Tunaweza kufa kwa njia ya ghafla, isiyo ya kutarajia ambayo itazuia maungamo ya mwisho. Chaguo pekee la busara ni kutubu na kumwamini Yesu Kristo leo. "Kwa maana asema, wakati uliokubalika nalikusikia, siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa" (2 Wakorintho 6: 2).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Biblia inasema nini kuhusu maungamo ya mwisho?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries