settings icon
share icon
Swali

Ni maneno gani saba ya mwisho ya Yesu Kristo msalabani, na yanamaanisha nini?

Jibu


Kuna haya saba ambazo Yesu Kristo alifanya juu ya msalaba (si kwa mpangilio wowote maalumu):

(1) Mathayo 27:46 inatuambia kwamba saa ya tisa Yesu alilia kwa sauti kuu, akisema, "Eloi, Eloi, lama sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?" Hapa , Yesu alikuwa akionyesha hisia zake za kuachwa, vile Mungu alivyoweka dhambi za ulimwengu juu yake — na kwa sababu hiyo, Mungu alipaswa 'kugeuka' kutoka kwa Yesu. Vile Yesu alihisi uzito wa dhambi, alikuwa anapitia utengano kutoka kwa Mungu kwa muda pekee katika milele yote. Hii pia ilikuwa kutimiza maneno ya kinabii katika Zaburi 22: 1.

(2) "Baba, wawasamehe, kwa maana hawajui walitendalo" (Luka 23:34). Wale waliomsulubisha Yesu hawakutambua upeo kamili wa yale waliyokuwa wakifanya kwa sababu hawakumtambua yeye kama Masihi. Ujinga wao wa ukweli wa Mungu haukumaanisha kwamba walistahili msamaha, na sala ya Kristo kati ya kumdhihaki Yake ni uonyesho wa huruma isiyo na kikomo ya neema ya Mungu.

(3) "Nakuambia ukweli, leo hii utakuwa pamoja nami katika paradiso" (Luka 23:43) Katika maneno haya, Yesu anahakikishia mmoja wa wahalifu msalabani kwamba atakapokufa, atakuwa pamoja na Yesu mbinguni. Hii ilitolewa kwa sababu, hata wakati wa kifo chake, mhalifu ameonyesha imani yake kwa Yesu, akimtambua kwa yule alikuwa (Luka 23:42).

(4) "Baba, mikononi mwako ninaweka roho yangu" (Luka 23:46). Hapa, Yesu anatoa moyo wake kwa hiari ndani ya mikono ya Baba, akionyesha kwamba alikuwa karibu kufa na kwamba Mungu alikuwa amekubali dhabihu yake. "Alijitolea Mwenyewe asiye na hatia kwa Mungu" (Waebrania 9:14).

(5) "Mwanamke mpendwa, hapa ni mtoto wako!" Na "hapa ni mama yako!" Yesu alipomwona mama yake amesimama karibu na msalaba pamoja na Mtume Yohana, ambaye alimpenda, aliweka huduma ya mama yake kwa mikono ya Yohana. Na tangu saa hiyo Yohana akamchukua nyumbani kwake (Yohana 19: 26-27). Katika aya hii Yesu, aliyekuwa Mwana wa huruma, anahakikisha kuwa mama yake wa kidunia anajaliwa baada ya kifo chake.

(6) "Nina kiu" (Yohana 19:28). Yesu hapa anatimiza unabii wa Kimasihi kutoka Zaburi 69:21: "Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki." Kwa kusema kwamba alikuwa na kiu, aliwahimiza walinzi wa Kirumi kumpa siki, ambayo ilikuwa ya kawaida katika kusulubiwa, na hivyo kutimiza unabii.

(7) "Imekwisha!" (Yohana 19:30). Maneno ya mwisho ya Yesu yalimaanisha kuwa mateso Yake yalikuwa yameisha na kazi yote Baba yake alimpa Yeye kufanya, ambayo ilikuwa ni kuhubiri injili, kufanya miujiza, na kupata wokovu wa milele kwa watu wake, ilifanyika, ilikamilishwa, kutimizwa. Deni la dhambi lililipwa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni maneno gani saba ya mwisho ya Yesu Kristo msalabani, na yanamaanisha nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries