settings icon
share icon
Swali

Je, malaika wana mabawa?

Jibu


Picha ya kawaida ya malaika kimsingi ni binadamu aliye na mabawa. Hii sio ya kibiblia. Mara nyingi Biblia huwawazilisha malaika kuonekana kama wanadamu. Hata hivyo, hii haionyeshi kuwa malaika katika asili yao wanafanana na wanadamu. Zaidi ya hayo, Biblia mara chache inaelezea malaika kuwa na mbawa. Hata hivyo, kuna dhahiri aina mbili za malaika waliotajwa katika Biblia ambao wana mbawa: makerubi (Kutoka 25:20; Ezekieli 10) na Serafi (Isaya 6). Makerubi na Maserafi ni aina mbili za malaika, labda maagizo mawili ya malaika. Hivyo, hii ni wazi, malaika wengine wana mbawa.

Biblia inatuambia kwamba malaika ni viumbe wa roho (Waebrania 1:14). Maelezo ya makerubi katika Ezekieli sura ya 10 na maserafi katika Isaya sura ya 6 ni ya kawaida sana. Ni wazi kwamba Ezekieli na Isaya walikuwa na shida kuelezea kwa usahihi maono ya kushangaza waliyoyaona ya mbinguni na malaika. Kama viumbe wa kiroho, haijulikani ni kwa nini malaika wangehitaji mbawa. Mtu wa roho hana haja ya mbawa ili kuruka. Malaika hawajafungwa na sheria za ulimwengu wa kimwili.

Kwa hiyo, malaika wana mabawa? Naam, malaika wengine wana mbawa. Hata hivyo, hatupaswi kupunguza kile ambacho malaika anaweza kufanya au hawawezi kufanya kulingana na uelewo wetu mdogo wa mbawa ambazo malaika wanazo kama ilivyoelezwa katika Biblia.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, malaika wana mabawa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries