settings icon
share icon
Swali

Malaika huonekana kama kama nini?

Jibu


Malaika ni viumbe wa roho (Waebrania 1:14), kwa hiyo hawana umbo lolote la kimwili. Lakini malaika wana uwezo wa kuonekana katika umbo la kibinadamu. Malaika alipoonekania wanadamu katika Biblia, walifanana na wanaume wa kawaida. Katika Mwanzo 18: 1-19, Mungu na malaika wawili walionekana kama wanaume na kwa kweli walikula chakula pamoja na Ibrahimu. Malaika huonekana kama mwanaume mara nyingi katika Biblia (Yoshua 5: 13-14; Marko 16: 5), na hawajaonekana kamwe kwa mfano wa kike.

Wakati mwingine, malaika hawakuonekana kama wanadamu, bali kama kitu kingine-kidunia, na kuonekana kwao kulikuwa na hofu kwa wale waliokutana nao. Mara nyingi, maneno ya kwanza kutoka kwa malaika hawa yalikuwa "usiogope," kwa sababu hofu ilikuwa hisia ya kawaida. Walinda kaburi la Yesu wakawa kama wafu walipomwona malaika wa Bwana (Mathayo 28: 4). Wafilisti katika mashamba katika Luka 2 walikuwa " na hofu kubwa" wakati malaika wa Bwana alipotokea na utukufu wa Bwana ukawazunguka.

Kwa ajili ya sifa za kimwili, wakati mwingine malaika huelezwa kama wenye mabawa. Sura za makerubi juu ya sanduku la agano zilikuwa na mabawa yaliyofunikwa kiti cha huruma (Kutoka 25:20). Isaya aliona Maserafi wenye mabawa katika maono yake ya kiti cha enzi cha mbinguni, kila mmoja akiwa na mabawa sita (Isaya 6: 2). Ezekieli, pia, aliona maono ya malaika wenye mabawa. Isaya 6: 1-2 inaonyesha malaika wana sifa za kibinadamu-sauti, nyuso na miguu. Sauti za malaika zinasikika zikiimba na kumsifu Mungu katika vifungu vingine kadhaa. Mojawapo ya maelezo kamili zaidi ya malaika ni katika Danieli 10: 5-6: "Nika macho, nikamwona mtu amevaa mavazi ya kitani na kiunoni amejifunga mkanda wa dhahabu kutoka Ufazi. Mwili wake ulingaa kama zabarajadi safi. Uso wake ulifanana na umeme, na macho yake yaliwaka kama miali ya moto. Miguu na mikono yake ilingaa kama shaba iliyosuguliwa sana. Sautiyake ilivuma kama sauti ya umati mkubwa wa watu." Malaika katika kaburi la Yesu alielezewa hivi: "Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji" (Mathayo 28: 3).

Njia yoyote malaika walichukua walipoonekana, kuna sababu ya kuamini kuwa hizo njia ni nzuri sana. Ezekieli anatuambia kwamba Lusifa "aliinuliwa" juu kwa kiburi cha urembo wake. Kwa kuongeza, viumbe kama malaika, ambao daima wako mbele za Mungu, watatarajiwa kuwa na urembo usio wa kawaida kwa sababu utukufu wa Mungu unaonekana juu ya wote waliyo karibu Naye.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Malaika huonekana kama kama nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries