settings icon
share icon
Swali

Je! Maana ya neno la Kiebrania upepo ni gani?

Jibu


Neno la Kiebrania ruaki linamaanisha, "pumzi" au "roho." Jina la mkabala la Kigiriki ni pumzi/roho. Maneno yote mawili ambayo yanatumika san asana katika vifungu hivi yanahusu Roho Mtakatifu. Utumikaji wa kwanza wa neno hili katika Biblia linaonekana katika aya ya pili: "Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji" (Mwanzo 1:2). Katika Mwanzo 6:17 neno roho limetafsiriwa na kumaanisha "pumzi ya uhai." Mwanzo 8:1 inatumia neno pumzi kuelezea "upepo" ambao Mungu alituma juu ya ardhi kuondoa maji ya ghalika. Kwa ujumla neno pumzi linapatikana karibu zaidi ya mara 400 katika Agano la Kale.

Mara nyingi wakati Agano la Kale linazungumzia juu ya "Roho wa Bwana" au Roho wa Mungu," neno linatumika kwa "Roho" ni pumzi. Umiaji wa neno pumzi kama "roho" lisipolinganishwa na Mungu mara nyingi linarejelea roho wa mwanadamu. Hii inaweza kumaanisha roho halisi wa mwanadamu (sehemu ya mwili inayofanana na moyo) au tabia ya mtu, hali ya hisia au hulika ya mtu. Roho kam "pumzi" au "upepo" inaweza maanisha pumzi ya kawaida au upepo, au ama inaweza chukua maana ya kimfano kama vile usemi safi wa kawaida "pumzi ya kawaida."

Pumzi ya Mungu ndio chanzo cha uhai. Pumzi ya Mungu ndiyo inapeana uhai kwa viumbe wote. Tunaweza kusema pumzi ya Mungu ndio imeumba kila kitu kinachoishi. Vitu vyote vinanvyoishi vina deni ya hiyo pumzi wanayopumua kwa Roho wa Mungu. Musa anakauli ukweli huu kwa wazi: "Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii" (Hesabu 27:16). Ayubu vile vile alielewa ukweli huu: "kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu" (Ayubu 27:3). Baadaye Elihu alimwambia Ayubu, "Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai" (Ayubu 33:4).

Mungu alitumia kifungu pumzi ya Yahweh katika ahadi yake kuwa Masihi atatiwa nguvu na Roho Mtakatifu: "Atainua bendera kwa mataifa na kuwakusanya Waisraeli walioko uhamishoni; atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika kutoka pembe nne za dunia" (Isaya 11:2; ona pia Isaya 42:1). Unabii huu ulitimizwa katika Yesu; katika ubatizo wake mto Yorodani, Yohana aliona "Roho wa Mungu akishuka kama njiwa na kutulia juu yake" (Mathayo 3:16).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Maana ya neno la Kiebrania upepo ni gani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries