settings icon
share icon
Swali

Mbona watu hufa?

Jibu


Watu hufa kwa sababu ya kile kinachoitwa "dhambi ya awali" -kuasi kwa Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni. Mungu alikuwa amewaonya wanadamu wa kwanza kwamba kutotii sheria yake ingeweza kusababisha kifo chao (Mwanzo 2:17), na ndivyo kilichotokea. "Mshahara wa dhambi ni kifo" (Warumi 6: 23a).

Adamu na Hawa walikuwa na nia ya kukaa na Mungu milele, hivyo labda hawakujua hata maana ya "kufa." Kwa bahati mbaya, dhambi iliingia eneo la mbinguni la malaika, na Shetani akamjaribu Hawa, na akaanguka katika dhambi. Hawa alimpa matunda mumewe, naye akamfuata katika dhambi. Dhambi hiyo ilileta kifo ulimwenguni, kwa kuwa watu walijitenga wenyewe kutoka kwa Chanzo cha Uzima.

Tangu wakati huo, kila mwanadamu aliyezalishwa na mwanamke kwa msaada wa mwanaume huzalisha watoto wenye dhambi. Hali hii ya dhambi huleta na kifo. "Dhambi iliingia ulimwenguni kwa njia ya mtu mmoja, na kifo kupitia dhambi, na kwa njia hii mauti alikuja kwa watu wote, kwa sababu wote walifanya dhambi" (Warumi 5:12).

Mwanzo 3 inaelezea laana ambayo Mungu alitangaza juu ya ulimwengu. Laana ni pamoja na maneno haya kwa Adamu: "hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi."(Mwanzo 3:19). Mungu alikua anazungumzia Kifo cha kimwili hapa. Kifo cha kimwili hakikutokea mara moja kwa Adamu na Hawa, lakini, kwa sababu ya dhambi yao, wanyama wasio na hatia walikufa (Mwanzo 3:21).

Aina nyingine ya kifo ambayo dhambi ya Adamu na Hawa ilisababisha ni kifo cha kiroho-roho zao zilitengana na Roho wa Mungu; ushirika wao ulivunjika. Kifo hiki cha kiroho kilitokea mara baada ya kula tunda waliyokatazwa na walikuwa na hofu na aibu (Mwanzo 3:10). Kifo cha kiroho, kama kifo cha kimwili, kiliendelea mpaka kwa kizazi chao (Waefeso 2: 1).

Tangu Adamu, jamii ya wanadamu imefanya kazi chini ya "sheria ya dhambi na kifo" (Warumi 8: 2). Mungu kwa wema wake alimtuma Mwanawe kukomesha sheria ya dhambi na kifo na kuanzisha "sheria ya Roho ambaye hutoa uzima" (Warumi 8: 2). Wakorintho wa Kwanza 15: 20-26 inasema, " Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. wa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa…. Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti. "

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mbona watu hufa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries