settings icon
share icon
Swali

Je! Kutosoma Biblia ni dhambi?

Jibu


Dhambi ni neno lolote, fikra, msukumo, au tendo ambalo limepungukiwa na "utukufu wa Mungu" (Warumi 3:23). Dhambi ni uvunjaji wa sheria ya Mung una uasi dhidi ya asili Yake na maagizo Yake. Ikiwa Mungu anakusudia tulisome Neno Lake, basi kukosa kulisoma ni dhambi.

Ukweli kwamba Mungu amevuvia Neno Lake na kulitunza katika karne zote inamaanisha kwamba Yeye anatamani lisomwe. Kwa nini akiandike kitabu ikiwa hakujali ikiwa watu watakisoma au la?

Dhambi huanzia moyoni, na hapo ndipo Mungu huangalia (1 Samweli 16: 7; Yeremia 17:10; Warumi 8:27). Ikiwa hatusomi Biblia kwa sababu hatuna haj ana kile ambacho Mungu amesema, tuna hatia ya kutojali. Ikiwa hatuisomi Biblia kwa sababu tunafikiria kuwa si lazima, tuna hatia ya kiburi. Ikiwa hatuisomi Biblia kwa sababu hatuwezi pata muda au hatuichukulii kuwa ya maana, tuna hatia ya kuwa na vipaumbele visivyo faa. Yesu alisema, "Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake" (Mathayo 6:33). Yesu pia alisema, "Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi" (Luka 12:48). Mungu anatutarajia tutumie wakati wetu, rasilimali, hisia kali, na huduma kwa kile kilicho na thamani ya milele.wale ambao wana Neno la Mungu katika vidole vyao wataulizwa chenye walifanyia hiyo bahati kubwa.

Katika Zaburi ya 119, ambayo inahusu Neno la Mungu, mtunga-zaburi "anajifunza," "anafikiria," "anatunza," "anatangaza," na "anatafakari" Neno la Mungu (Zaburi 119: 6-8, 13, 15). Vitendo hivi vyote hutumia vibaya usomaji wa Biblia. Na sio kusoma tu, bali hamu ya dhati ya kujua Neno la Mungu, kulitumia maishani, na kulishiriki na wengine.

Zaidi ya mfano wa mtunga-zaburi, muumini anaambiwa "Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli" (2 Timotheo 2:15). Kwa agizo hili la moja kwa moja la kulisoma Neno, inaonekana kuwa kutosoma neno ni dhambi.

Kulisoma na kulitafakari Neno la Mungu kunatuandaa kuweza kushughulikia kwa ufasaha changamoto za maisha ili kuepuka dhambi ya kutojua (ya kutosoma Biblia) na tunaweza kuzuia dhabi ya makusudi: "Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi" (Zaburi 119:11). Kuisoma Biblia huchangia katika ukuaji wa kiroho (1 Petro 2:2).

"Kwa maana Neno la Mungu li hai tena lina nguvu. Lina makali kuliko upanga wowote wenye makali kuwili, hivyo linachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, viungo na mafuta yaliyo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo" (Waebrania 4:12). Sisi sote tunahitaji uchunguzi wa Neno la Mungu katika maisha yetu. Tunahitaji kusoma Biblia kila wakati.

Wakristo wana jukumu la kujua Neno la Mungu ili waweze kulielezea kwa ufasaha kwa ulimwengu. Petro wa Kwanza 3:15 anatuamuru kuwa tuwe tayari kila wakati ili kutoa jibu juu ya tumaini tulilonalo katika Kristo. Wasio Wakristo wana maswali. Wanapokutana na Mkristo ambaye hajui Biblia vizuri, inaweza kuonekana kuwa hakuna majibu, na hili ndio dharau la wale walio na maswali.

Kwa watu wengi, Biblia inapatikana kwa urahisi katika njia nyingi. Ni dhambi kupuuza nafasi zetu za kusikia kutoka kwa Mungu. Kwa wanafunzi wasiojua kusoma na wale wakusikia sauti tu, Bibilia za sauti zinapatikana. Bibilia za kujifunza zimejazwa na maoni ya kutusaidia kuelewa vifungu vigumu. Matoleo ya kisasa na fafanusi husaidia hali za zamani kuwa hai ili tuielewe Biblia katika muktadha wake wa kweli. Yakobo 4:17 inaweza kutumika katika kusoma Biblia: "Basi mtu yeyote anayejua jema limpasalo kutenda, lakini asilitende, mtu huyo anatenda dhambi."

Mara nyingi tunajishughulisha kuwa ikiwa jambo fulani ni dhambi, huwa tunauliza swali lisilofaa. Swali linalowafaa Wakristo ni hili: "Je! Yesu angependa nifanye nini? Katika maombi yake marefu yaliyonakiliwa, Yesu alimuuliza Baba "Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli" (Yohana 17:17). Sasa tunalo jibu Lake. Anataka tutakasike, na tunaweza kutafuta hilo kwa kulisoma na kuliweka katika matumizi Neno la Mungu. Kuipuuza Biblia ni chukizo kwake na inatufanya tuwe hatarini udanganyifu wa ule adui wetu, Shetani (1 Petro 5:8).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Kutosoma Biblia ni dhambi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries