settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kuwa mtoaji wa furaha zaidi?

Jibu


Tunaweza kujifunza kuwa watoaji wenye furaha kwa kujifunza kuhusu mtoaji mkuu duniani ambaye amewahi kujulikana: Yesu Kristo. Huku akiacha nyuma utajiri na utukufu wa Ufalme wake wa mbinguni, alikuja duniani na kwa hiari alitoa uhai wake ili tuweze kuwa na uhai wetu. Kama Mungu alivyowaandalia watoto Wake kuwa sawa na mfano wa Mwanawe (Warumi 8:29), hakuwezi kuwa na njia nyingine bora zaidi ya kumwiga Yesu Kristo kuliko kwa kujitolea bila kujipenda jinsi alivyo fanya. Mwokozi wetu mwenyewe alituambia, "Ni heri kutoa kuliko kupokea" (Matendo 20:35). Kwa hiyo, basi, msukumo wetu mkubwa kwa kutoa kwa furaha na ukarimu lazima uwe ni kumpendeza Bwana na kuonyesha zawadi yake ya wokovu kwetu.

Barua ya pili kwa Wakorintho inafunua kweli nyingi za msukumo ambazo zinapaswa kutusaidia kuwa watoa kwa furaha zaidi. Kama Paulo aliwahimiza Wakorintho kwa hekima, "Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu" (2 Wakorintho 9: 6). Ukweli huu usioeleweka pia ulielezwa na Sulemani miaka elfu moja kabla: " Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya... " (Mithali 3: 9-10). Na Kristo mwenyewe alituambia, "Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu... " (Luka 6:38). Hakika, "Mema yatakuja kwake mwenye ukarimu ..." (Zaburi 112: 5).

Kanuni hii hakika ii wazi kabisa-hatuwezi kutoa kumliko Muumba wetu mwenye neema. Tunapojitolea zaidi katika huduma kwa Bwana, pia yeye ataturejeshea. Kwa kweli, mahali pekee katika Biblia ambako Mungu anatualika tumjaribu Yeye ni Malaki 3:10 ambayo inasema juu ya sadaka zetu zilizotolewa kwake: "... mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la." Mara nyingine, maneno ya Sulemani yanasema hivi: "Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji. Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa; Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe" (Methali 11: 24-25).

Kama Paulo alivyosema, "Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu" (2 Wakorintho 9: 7). Kutoa kwa furaha, kwa hiyo, lazima kuwe njia ya maisha kwa Mkristo ambaye anaelewa neema ya Mungu. Tunapotoa kwa ukarimu na kwa moyo unaotamani, Mungu anatuhakikishia kuwa atatulinda na kututunza (Isaya 58: 9, Zaburi 41: 1-3, Mithali 22: 9; 2 Wakorintho 9: 8, 11). Na tunahitaji kukumbuka kwamba sio fedha zetu pekee ambazo tunapaswa kutoa kwa Mungu kwa furaha. Kama Mfalme Daudi alivyosema, kila kitu tulicho nacho ni cha Mungu (1 Mambo ya Nyakati 29:14), na hii inajumuisha vipaji vyetu na wakati wetu pia. Kama siku zetu zimehesabiwa (Zaburi 139: 16), wakati wetu kweli ni wa Mungu. Na zawadi yoyote tunayo pia ni kutoka kwake; Kwa hiyo, "kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu" (1 Petro 4:10).

Ni jinsi gani Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa (Yohana 3:16). Tunapaswa kukumbuka kwamba tunaokolewa kwa sababu Mungu wetu alitoa kwa ukarimu. Kama watoto wake, tunaitwa kuwa "mwanga wa ulimwengu" (Mathayo 5:14). Tunapomtumaini Mungu na kumheshimu kwa kutoa kwa wakati wetu, hazina, na talanta, tunaruhusu mwanga wetu kuangaza mbele ya wanadamu, na wema wetu utangaa kwa Baba yetu mbinguni.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kuwa mtoaji wa furaha zaidi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries