settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu kutahiriwa? Mtazamo wa Kikristo ni upi kuhusu kutahiriwa?

Jibu


Kutahiriwa ni upasuaji wa kuondoa kwa mzunga, au kiungo, cha kiume. Neno la kutahiri maana halisi linamaanisha "kukata." Kama utamaduni wa dini, kutahiriwa kulihitajika kwa uzao wote wa Ibrahimu kama ishara ya agano Mungu alifanya pamoja naye (Mwanzo 17: 9-14, Matendo 7: 8). Sheria ya Musa ilirudia hitaji hilo tena (Mambo ya Walawi 12: 2-3), na Wayahudi katika karne zote wameendelea kutahiriwa (Yoshua 5: 2-3, Luka 1:59, Matendo 16: 3; Wafilipi 3: 5). Kuna masuala mbalimbali yanayohusika katika swali la ikiwa wanaume hii leo wanapaswa kutahiriwa au la. Suala moja ni mafundisho ya kidini: Biblia, Neno la Mungu, inasema nini? Suala jingine ni, la afya, wanaume wanapaswa kutahiriwa? Mtazamo wa Kikristo wa kutahiriwa labda utaelezewa bora ikiwa maswala yote mawili yatawekwa pamoja.

Kuhusu suala la kwanza, Wakristo wa Agano Jipya hawako chini ya sheria ya Agano la Kale, na kutahiriwa hakufai tena. Hii inadhihirishwa katika vifungu kadhaa vya Agano Jipya, kati ya hizo ni Matendo 15; Wagalatia 2: 1-3; 5: 1-11; 6: 11-16; 1 Wakorintho 7: 17-20; Wakolosai 2: 8-12; na Wafilipi 3: 1-3. Vile vifungu hivi vinatangaza, kuokolewa kutoka kwa dhambi zetu ni matokeo ya imani katika Kristo; ni kazi ya Kristo iliyokamilika msalabani inayookoa, sio utunzaji wa tamaduni. Hata Sheria ilikubali kwamba kutahiriwa peke yake hakukuwezesha kumpendeza Mungu, ambaye alielezea haja ya "tahiri mioyo yenu" (Kumbukumbu la Torati 10:16; tazama Warumi 2:29). Katika wokovu, kazi za mwili hazifanyi chochote (tazama Wagalatia 2:16).

Katika Matendo 16: 3, Paulo alikuwa na msaidizi wa umisionari, Timotheo, aliyetahiriwa. Timotheo alikuwa nusu ya Myahudi, na Paulo alimtahiri ili asiweze kuwa kizuizi jinsi walitafuta kufikia Wayahudi wasiookoka. Ingawa Mungu hakumtaka Timotheo atahiriwe, ilikuwa kitu alichofanya kwa hiari kwa kuwafikia Wayahudi. Hata hivyo, kama vile Paulo anasema kwa uwazi katika Wagalatia, kutahiriwa hakusaidii katika wokovu au utakaso ndani ya Kristo. Bila shaka, tukio hilo na Timotheo halitumiki moja kwa moja hii leo kwa sababu Wakristo hawapaswi kutahiriwa ili kuwafikia wasioamini, iwe Wayahudi au Wayanani. Mara nyingine tena, kanuni ya kutahiriwa kwa moyo ni kuu.

Kuna masuala ya vitendo yaliyohusisha kutahiriwa pia. Baadhi ya wazazi wamepata wanao kutahiriwa ili waweze kuonekana kama wanaume wengine wote katika utamaduni wao. Wazazi wengine wana wasiwasi kwamba siku moja mtoto wao atakuwa katika chumba cha kujifungia na kujipata tofauti na kila mtu mwingine. Hata hivyo, katika tamaduni fulani, wanaume hawakatahiriwa. Kuna suala la afya. Madaktari wanajadiliana mbele na nyuma kuhusiana kama kuna faida yoyote ya afya ya kutahiriwa. Wazazi wote wenye wasiwasi huo wanapaswa kuzungumza na daktari kuhusu suala hili.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu kutahiriwa? Mtazamo wa Kikristo ni upi kuhusu kutahiriwa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries