settings icon
share icon
Swali

Je! Ni nani ameidhinishwa kusimamia Meza ya Bwana?

Jibu


Wakristo ulimwenguni wanakubaliana kwamba Meza ya Bwana ilianzishwa na Kristo na inapaswa kuzingatiwa kama sheria kanisani na wafuasi Wake. Ilikuwa kwa kanisa la Korintho ambao Paulo aliwaandikia maagizo kuhusu Meza ya Bwana (1 Wakorintho 11: 23-26). Baadaye Paulo alimwandikia Timotheo juu ya sifa za viongozi wa kanisa, maaskofu / wazee na mashemasi (1 Timotheo 3: 1-13). Katika lugha ya asili, neno "shemasi" linatokana na kitenzi kinachomaanisha "kutumikia," labda kwa maana ya kuandaa meza, lakini pia ilitumika kuashiria huduma anuwai kanisani. Kwa sababu ya kidokezo cha huduma ya mezani katika neno "shemasi" na utovu wa Meza ya Bwana katika ibada ya kanisa la kwanza, kuna dalili kubwa kwamba kutumikia viashiria vya ushirika ilikuwa kazi maalum ya mashemasi.

Kutokana na haya tunaweza kutamatisha kuwa uongozi wa kanisa ulitengwa kwa ajili ya kuongoza Meza ya Bwana katika kanisa la kwanza; walakini, hamna maandiko hasa yenye maagizo ya "jinsi" ya kufanya. Kwa hivyo, inaweza onekana bora kwa uongozi, ikiwa hamna mashemasi wa kutosha katika ibada, kuchagua watu wa kawaida kutumikia katika Meza ya Bwana.

La muhimu zaidi kuliko anayehudumia katika Meza ya Bwana ni tabia ambayo anayetumika na yule anayepokea. Wakorintho wa Kwanza 11:27 inasema kwamba wale wanaochukua mwili kwa njia "isiyofaa" wana hatia ya dhambi dhidi ya mwili na damu ya Kristo. "Njia isiyostahili" inaweza kumaanisha kuchukua mwili na wale ambao sio wa Kristo au kuzichukua kwa njia ya kiupumbavu au isiyo na heshima. Inaweza kumaanisha pia kutumia sherehe kama njia ya kuonekana mbele ya watu ili wakusifu. Mstari wa 28 unatoa vigezo vya kutumikia na kushiriki katika Meza ya Bwana. Tunapaswa kujichunguza kabla ya kula na tuhakikishe mioyo yetu iko sawa mbele za Bwana. Halafu wote, wanaotumikia na wapokeaji wanaweza kuwa na hakika ya kumpendeza Mungu wanaposhiriki katika ushirika Wake mtakatifu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Ni nani ameidhinishwa kusimamia Meza ya Bwana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries