settings icon
share icon
Swali

Je, kuomba kwa maandiko kuna ufanisi zaidi kuliko sala nyingine?

Jibu


Watu wengine wamegundua kwamba kunukuu mistari ya Biblia katika sala zao ni njia ya kuomba yenye ufanisi. "Kuomba Mungu kwa Maandiko" inaonekana kusaidia kuzingatia kwa akili na kuhakikishia kwamba jambo linaaloombewa inampendeza Mungu.

Yakobo 5:16 inasema, "...Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. ." Yohana wa Kwanza 5: 14-15 inasema, " Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba. . "Neno 'ufanisi' linamaanisha" inatosha kuzalisha matokeo yaliyohitajika. "Kwa bidi hapa ina maana" mara kwa mara, yenye makali.'' Yakobo na Yohana wote wanatuambia kwamba kwa maombi yetu kuwa yenye ufanisi, lazima yawe yenye nguvu, yenye maana, yenye kubaliana na mapenzi ya Mungu.

Njia moja ya kujua kwamba sala zetu zinampendeza Mungu ni kuomba kwa Maandiko maalum ambayo yanaonyesha yaliyo ndani ya mioyo yetu. Maandiko haipaswi kutumiwa kama aina fulani ya maneno ya uchawi, kurudia bila kutilia maanani kana kwamba maneno yenyewe yalikuwa na nguvu. Nguvu ya sala hutoka kwa Mungu peke yake kwa moyo "wenye bidii." Lakini tunapopata amri au ahadi inayoonyesha yaliyo ndani ya mioyo yetu, tunajua tunakubaliana na Mungu tunapoitumia kama sala. Ni Neno Lake. Tunapoweza kukumbua na kutafakari Zaidi juu ya Biblia, inakuwa sehemu yetu. Ukweli tuliojifunza huja akilini wakati tunapoomba na mara nyingi ni jibu tunayotaka. Mara nyingi, wakati hatujui nini cha kuomba, Maandiko yanaweza kutupa maneno. Zaburi ina mamia ya sala, ambazo tayari zimeweka mawazo yetu kuwa maneno.

Yesu anatoa mfano wetu bora wa sala ya ufanisi. Sala yake ndefu katika kumbukumbu zaidi ni "Sala yake ya Kuhani Mkuu," inayopatikana katika Yohana 17. Kitu cha kwanza tunaona ni umoja anao Roho wa Yesu na Baba. Anaanza kwa kusema, "Baba, saa imekwisha kufika." Yesu hakumwambia Baba chochote ambacho hakujua. Badala yake, Yesu alikuwa akikubali kwamba walikuwa wamekubaliana. Alitumia muda mwingi katika sala hivi kwamba alijua moyo wa Baba. Hiyo ndiyo lengo la maombi ya kweli: kuelewa moyo wa Mungu na kufanya mapenzi yetu sawia na Yake. Ikiwa kwa kutumia maneno yetu wenyewe au yale yaliyoandikwa miaka elfu mbili iliyopita, muhimu katika maombi yenye ufanisi ni kwamba hutoka kwa moyo na hutafuta mapenzi ya Mungu.

Kuomba kwa Maandiko kama tendo la kujitolea binafsi ni njia nzuri ya kujua tunaomba kwa usahihi. Kwa mfano, tunaweza kuchukua Wagalatia 2:20 na kuitumia kama sala ya kutakasa. Sala kama hiyo inaweza kusikia kuwa hivi: " Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu. " Katika kuomba kwa njia hii, tunafanya moyo wake Mungu kuwa lengo letu. Hakuna sarakasi katika maneno hayo, lakini tunaweza kujua tunaomba kulingana na mapenzi ya Mungu tunapotumia Neno Lake kama mfano.

Lazima tuwe makini tusichukulie Maandiko kama kwamba kila kifungu kiliandikwa hasa kwa hali yetu. Hatuwezi nukuu mstari ya Maandiko tu kwa sababu tunataka iwe ya kweli kwetu. Kwa mfano, Mungu aliahidi Solomoni "utajiri, mali, na heshima" katika 2 Mambo ya Nyakati 1: 11-12. Lakini hatuwezi kuomba kwa huo mstari kana kwamba Mungu alituahidi sisi. Hatuwezi kutafuta mistari pekee ambayo inasema tunachotaka iseme na kisha "kuidai". Kuna nyakati, hata hivyo, wakati Mungu anaweka mstari ya Maandiko fulani kwenye mioyo yetu kama ujumbe wake binafsi kwetu, na tunaweza na tunapaswa kuomba juu yake.

Ikiwa tunajaribu kutumia kila mstari kama kwamba imeathiri moja kwa moja maisha yetu wenyewe, tutaweza kuwa na tatizo na mistari kama 1 Samweli 15: 3: " Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, ... " Tunapaswa tu kusoma Maandiko katika muktadha wake na kujifunza zaidi kuhusu Mungu kutokana na kanuni tunazozipata. Mungu anaweza kutumia kifungu hicho kutuzungumzia kuhusu kuharibu kabisa utamaduni katika maisha yetu. Katika hali hiyo, tunaweza kuomba, "Bwana, kama ulivyowaambia Waisraeli kuharibu kabisa kila kitu kilichowakilisha mabaya ya Waamaleki, nataka kuvunja miungu yoyote ya uwongo katika maisha yangu na kuondoa chochote kile isipokuwa Wewe tu. Utakase moyo wangu kama walivyoitakasa nchi yao. "

Maombi yenye ufanisi yanaweza kutoka kwa Maandiko au kutoka kwa kina cha mioyo yetu wenyewe. La muhimu tunapokua kiroho ni haya yapate kuingiliana. Hata juu ya msalaba katika mateso mabaya, Yesu alitoa sauti kutoka Zaburi ya 22: "Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?" Wanachuoni wengi wanaamini kwamba alikuwa anukuu kifungu hicho kama alipokuwa akipigwa msalabani, akiomba Mungu kama tendo la ibada hata katika kifo. Tunavyojifunza na kuyabinafsisha maandiko zaidi, sala zetu zitakuwa sawia na mapenzi ya Mungu na zitakuwa na ufanisi zaidi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, kuomba kwa maandiko kuna ufanisi zaidi kuliko sala nyingine?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries