settings icon
share icon
Swali

Ni kwa nini kumngojea Mungu ni jambo gumu sana?

Jibu


Kumngojea Mungu sio jambo ngumu tu; bali wakati mwingine inaonekana jambo ambalo lisilowezekana. Tunataka mambo kufanyika wakati wetu wenyewe, na kulingana na mipango yetu wenyewe. Lakini Mungu hafanyi kazi kwa mjibu wa mpangilio wetu, na tunapotarajia kwamba Yeye atatende huwa tunakata tamaa. Mungu ana mtazamo mkubwa zaidi wa matukio katika maisha yetu, na mtazamo wake, mipango, na utaratibu wak uu kamili na takatifu, kwa sababu Yeye ni mkamilifu na mtakatifu. Mtunga zaburi anatuambia "Njia ya Mungu ni kamilifu" (Zaburi 18:30). Ikiwa njia za Mungu ni "kamilifu," basi tunaweza kuamini kwamba chochote afanyacho-na wakati wake ufaao pia ni kamilifu. Tunapofikia uelewo wa ukweli huu, kumngojea Mungu halitakuwa jambo gumu sana kufanya, bali kutabadilka na kuwa furaha.

Ahadi za Mungu ziko wazi kwa suala hili — ikiwa tutamngojea Mungu, atafanya upya nguvu zetu (Isaya 40:31). Lakini sisi ni wanadamu na tunaishi katika mila ambao unahitaji kila jambo lifanyike sasa hivi au mapema kama jana. Ndio maana kumngojea Mungu itakuwa ngumu. Wakati mwingine, sala tunazozileta kwa Bwana wa Majeshi zitajibiwa mara hiyo hiyo, na hiyo inatutia nguvu kuendelea kuamini na kuwa na ujaziri. Hata hivyo, muda mwingine, Bwana huijaribu imani yetu, na huo ndio wakati ule sisi hutatizika. Na huo ndio wakati mambo yanaweza kuwa magumu na ndio wakati huwa tunajiuliza ikiwa kweli Bwana anasikia maombi yetu.

Katika himizo la mtume Paulo kwa kanisa la Filipi anawasii wasiwe na wasiwasi juu ya chochote (Wafilipi 4: 6). Toleo la Mfalme Yakobo (King James version) linaitafsiri kuwa tunapaswa kuwa, "tunafaa kuwa macho kwa kila jambo." Hii inamaansiha hatustahili kuwa makini kwa kila kitu na kusumbuliwa na kitu chochote ambacho ni cha haja. Woga ndani ya muumini inaashiria kwamba kuna ukosefu wa Imani na hiyo humhushunisha Mungu, sio kwa sababu hataki tuwe na wasiwasi kwa chochote, ni kwa sababu anajua hofu yetu inatokana na ufahamu ambao haujakamilika wa kuwa yeye ni nani.

Sehemu muhimu katika asili ya Mungu na tabia na maadili ambazo zitatuwezesha kumungojea kwa uvumilivu and uhakika kamili ni Ukuu wake. Ukuu wa Mungu umefafanuliwa kuwa udhibiti wake kamili kwa kiumbe, tukio na hali kwa kila wakati wa historia. Hawajibiki kwa mtu yeyote wala kushawishiwa na mtu yeyote, kamwe yeye anajitegemea, Mungu hutenda chenye anafurahishwa nacho kadri na vile anavyopenda, na hakuna chochote kitakacho mzimamiza: "nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote" (Isaya 46:10). Pindi tunapota ufahamu huu, kumugojea Mungu wetu mkamilifu kutenda katika wakati wake ufaao haituwezeshi kumngojea Mungu kwa uvumilivu pekee, bali pia huturuhusu kungojea kwa ujasiri.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni kwa nini kumngojea Mungu ni jambo gumu sana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries