settings icon
share icon
Swali

Ji! Ina maana gani kumfundisha mtoto katika njia impasayo?

Jibu


Ushauri wa Sulemani kwa wazazi ni "mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee" (Mithali 22:6). Kulea na kumfundisha mtoto katika muktadha wa methali hii inamaanisha kwamba inanza na Biblia, kama "kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya ..." (2 Timotheo 3:16). Kuwafundisha watoto ukweli wa Maandiko utawafanya wawe wenye busara kwa ajili ya wokovu (2 Timotheo 3:15); kuwawezesha kabisa kufanya kazi nzuri (2 Timotheo 3:17); watayarishe kutoa jibu kwa kila mtu anayewauliza sababu ya tumaini lao (1 Petro 3:15); na watayarishe kuhimili shambulio la tamaduni linalo uwezo katika kuwafundisha vijana wenye maadili ya kidunia.

Biblia inatuambia kwamba watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu (Zaburi 127:3). Kwa hakika inaonekana kustahili, basi, kwamba tusikize shauri la hekima la Sulemani la kuwafundisha kwa usahihi. Kwa kweli, thamani ambayo Mungu aliweka katika kufundisha watoto wetu ukweli linashughulikiwa kwa wazi na Musa ambaye alisisitiza kwa watu wake umuhimu wa kuwafundisha watoto wao kuhusu Bwana na amri na sharia Zake: "Nawe uwafundishe watoto wako kwa bidi, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako"(Kumbukumbu la Torati 6:7-9). Ukamilifu wa Musa unasisitiza wasiwasi wake mkubwa kwamba vizazi vilivyofuata vinaendelea kutii sheria za Mungu ili kuhakikisha kwamba "wataishi salama katika nchi" (Mambo ya Walawi 25:18), kwamba yote "yataenda vizuri" nao (Kumbukumbu la Torati 12:28), na kwamba angewabariki katika nchi (Kumbukumbu la Torati 30:16).

Maandiko inafundisha wazi kuwa kuwafunza watoto kumjua na kumtii Mungu ni msingi wa kumpendeza Yeye na kuishi kwa ushindi katika neema Yake. Kumjua Mungu na ukweli Wake huanza na ufahamu wa mtoto kuhusu dhambi na haja yake ya Mwokozi. Hata watoto wachanga sana wanaelewa kuwa wao sio wakamilifu na wanaweza kushika katika umri mdogo haja ya msamaha. Wazazi wanaopenda ni mfano wa Mungu mwenye upendo ambaye sio tu anasameha, bali hutoa sadaka kamili ya dhambi katika Yesu Kristo. Kufundisha watoto katika njia iwapasayo inamaanisha, kwanza kabisa, kuwaelekeza kwa Mwokozi.

Adhabu ni sehemu muhimu ya kulea watoto wa kumcha Mungu, kwa maana tunajua kwamba "Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi" (Mithali 3:12). Kwa hiyo, hatupaswi kuchukua nidhamu kimsaha wala tusivunjike mioyo kwa kuwa Bwana "naye humpiga kila mwana amkubaliye" (Waebrania 12:5-6). Na tunajua kwamba Mungu hutuadhibu kwa faida yetu, ili tuweze kushiriki katika utakatifu Wake (Waebrania 12:10). Vivyo hivyo, tunapowaadhibu watoto wetu, wanapokea hekima (Mithali 29:15) na watatuletea amani (Mithali 29:17) na heshima (Waebrania 12:9). Kwa hakika, hata watoto wachanga wanaweza kutambua kwamba nidhamu inatokana na upendo. Ndiyo sababu watoto wanaokua katika familia bila nidhamu mara nyingi huhisi kuwa hawapendwi na wana uwezekano mkubwa wa kutotii mamlaka wakati wanapokua wazima. Kumbuka kwamba nidhamu inayotolewa inapaswa kuwa sawa na kosa. Nidhamu ya kimwili, kama vile kutandika matakoni (kuhamasishwa vizuri), inapuuzwa na Biblia (Mithali 13:24, 22:15, 23:13-14). Hakika nidhamu, ingawa inaweza kuonekana haifai wakati inapokelewa, itazalisha "lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani" (Waebrania 12:11).

Wazazi wanapaswa kuwa na ari sawa kwa kuwafundisha watoto wao ambayo Musa alifanya. Wazazi wamepewa haki ya kuwa watumishi wa maisha ya watoto wao kwa muda mfupi sana, lakini mafundisho na mafunzo wanayotoa ni ya milele. Kwa mujibu wa kanuni za Mithali, mtoto ambaye amefunzwa kwa bidii katika "njia impasayo" atakuwa bado wa kweli kwa njia hiyo katika maisha haya na atavuna mafanikio yake katika ijayo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ji! Ina maana gani kumfundisha mtoto katika njia impasayo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries