settings icon
share icon
Swali

Je, Biblia inasema nini kuhusu kulea watoto?

Jibu


Mungu aliumba familia. Mpango Wake ulikuwa kwa mwanamume na mwanamke kuoana milele na kuwalea watoto kumjua na kumheshimu Yeye (Marko 10:9; Malaki 2:15). Kuasili pia ni wazo la Mungu, na Yeye huonyesha mfano huu katika kutuasili sisi kama watoto Wake (Warumi 8:15, 23; Waefeso 1:5). Bila kujali njia ambazo wanaingia katika familia, watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu na anajali jinsi wanavyolelewa (Zaburi 127:3, 34:11; Mithali 23:13-14). Wakati Mungu anatupa zawadi, pia anatoa maagizo ya wazi kuhusu matumizi yao.

Wakati Mungu aliwaongoza Waisraeli kutoka utumwa, aliwaagiza kuwafundisha watoto wao yote aliyowafanyia (Kumbukumbu la Torati 6:6-7; 11:19). Alipenda kuwa vizazi vijavyo viendelee kutekeleza amri Zake zote. Wakati kizazi kimoja kinashindwa kuingiza sheria za Mungu katika kijayo, jamii hupungua haraka. Wazazi hawana tu wajibu kwa watoto wao, bali ni kazi kutoka kwa Mungu ili kuwaarifu maadili na ukweli Wake katika maisha yao.

Maeneo kadhaa katika Maandiko hutoa maagizo maalum kwa wazazi kuhusu jinsi ya kulea watoto wao. Waefeso 6:4 inasema, "Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana." Kuna njia kadhaa ambazo wazazi wanaweza kuwachokoza watoto wao kwa hasira. Baadhi ya wazazi huweka viwango visivyowezekana ili mtoto akate tamaa ya kuitimiza kamwe. Wazazi wengine huwasumbua, huwadhihaki, au huwadhalilisha watoto wao kama njia ya adhabu, ambayo haina chochote bali huwachokoza kuwa hasira. Ukinzani pia kunaweza kufanya hasira kwa kuwa mtoto hana uhakika kamwe juu ya matokeo ya matendo yake. Unafiki huwafanya watoto kukasirika wakati wazazi wanahitaji tabia kutoka kwa watoto ambayo wazazi hawajichagulii wenyewe.

Ili "kuwalea katika adhabu na maonyo ya Bwana" inamaanisha kuwa wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao jinsi Mungu anavyotufundisha. Kama Baba, Mungu "si mwepesi wa hasira" (Hesabu 14:18, Zaburi 145:8), mvumilivu (Zaburi 86:15), na wa kusamehe (Danieli 9:9). Adhabu yake imekusudiwa kutuleta kwa toba (Waebrania 12:6-11). Maonyo Yake hupatikana katika Neno Lake (Yohana 17:17, Zaburi 119:97), na anataka wazazi kujaza nyumba zao na ukweli Wake (Kumbukumbu la Torati 6:6-7).

Pia anawaadhibu watoto Wake (Mithali 3:11, Waebrania 12:5) na anatarajia wazazi wa kidunia kufanya hivyo (Mithali 23:13). Zaburi 94:12 inasema, "Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, na kumfudisha kwa sharia yako." Neno adhabu hutoka kwa mzizi wa neno mwanafunzi. Kumwaadhibu mtu kuna maana ya kumfanya mwanafunzi. Adhabu ya Mungu imekusudiwa "kutufananisha na mfano wa Kristo" (Warumi 8:29). Wazazi wanaweza kufanya wanafunzi wa watoto wao kwa kufundisha maadili na masomo ya maisha waliyojifunza. Kama wazazi wanavyoishi maisha ya kumcha Mungu na kufanya maamuzi ya kudhibitiwa na Roho (Wagalatia 5:16, 25), wanaweza kuwatia moyo watoto wao kufuata mfano wao. Adhabu sahihi, thabiti huleta "mavuno ya haki" (Waebrania 12:11). Kushindwa kuadhibu husababisha aibu kwa mzazi na mtoto (Mithali 10:1). Methali 15:32 inasema kwamba mtu asiyejali nidhamu "hujidharau mwenyewe." Bwana alimhukumu Eli kuhani kwa sababu aliruhusu wanawe kutomheshimu Bwana na "kushindwa kuwazuia" (1 Samweli 3:13).

Watoto ni "urithi kutoka kwa Bwana" (Zaburi 127:3). Anawaweka katika familia na huwapa wazazi mwongozo wa jinsi watakavyolelewa. Lengo la uzazi mzuri ni kuzalisha watoto wenye busara ambao wanamjua na kumheshimu Mungu na maisha yao. Mithali 23:24 inaonyesha matokeo ya mwisho ya kulea watoto kulingana na mpango wa Mungu: "Baba yake mwenye haki atashangilia; naye amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia."

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Biblia inasema nini kuhusu kulea watoto?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries